Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Asilimia kumi ya bajeti ya Halmashauri nchini hutengwa kwa ajili ya mikopo ya vijana na wanawake. Je, Serikali ina mkakati gani wa kusimamia fedha hizo zitolewe kwa kila Halmashauri?

Supplementary Question 1

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, kwa kuwa asilimia kumi iliyopo sasa hivi imepitwa na wakati, na wanawake na vijana wanakuwa kwenye makundi ya watu watano, watano, wanagawana hiyo asilimia 10 wanagawana shilingi laki moja, pesa ambayo haiwezi kukidhi matakwa ya mahitaji yao. Je, serikali ina mpango gani wa kuongeza asilimia kumi iliyoko sasa hivi? (Makofi)
Swali la pili, kwa kuwa asilimia kumi iliyoko sasa hivi haitoki kwa wakati na wakati mwingine inasubiri matukio muhimu kama vile Mwenge. Je, ni lini Serikali itafanya sasa asilimia hii itoke kwa wakati?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Bupe, kwa sababu nimeona akiguswa sana na kinamama na vijana katika maeneo yake. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge hiyo ni credit kwako, kwa sababu naona unawatumikia wananchi wako wa Mkoa wa Rukwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema awali asilimia kumi ni mgao katika mapato ya ndani, na asilimia kumi hii inatofautiana kutoka Halmashauri moja na kwenda Halmashauri nyingine. Kwa mfano, Halmashauri ambayo collection yake kwa mwezi ni shilingi milioni 200, unapozungumzia asilimia kumi maana yake unazungumzia shilingi milioni 20. Lakini tujue kwamba kiwamba kiwango hiki ni (own source) mapato ya ndani ya Halmashauri, na katika yale mapato ya ndani kuna mgawanyiko wa aina mbalimbali kutoka mapato ya ndani, kuna mingine kutoka miradi ya maendeleo, kuna vitu mbalimbali. Kwa hiyo, hii asilimia kumi kiundani ni asilimia yenye kutosha kabisa katika mchakato wa own source, kwa sababu ile pesa ya ndani bado kuna mahitaji mengine ya miradi ya maendeleo inatakiwa ifanyike katika Halmashauri.
Kwa hiyo, hii asilimia kumi siyo ndogo, isipokuwa lengo kubwa ni kila Halmashauri iweze kujipanga ikusanye mapato ya kutosha kutoka katika vyanzo vya ndani. Kuna Halmashauri zingine kwa mwezi wanakusanya shilingi milioni 500, asilimia kumi ni shilingi milioni 50; ni imani yangu kubwa kama kila Halmashauri imejipanga vizuri wanapofanya collection zao mfano hata shilingi milioni100, asilimia kumi yake ni shilingi milioni kumi, wakiamua kuzigawa zile vizuri, wakipanga mpango mkakati vizuri, zitawasaidia kina mama na vijana katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo letu kubwa lilikuwa pesa tulizozipanga katika own source ten percent ilikuwa haiendi kwa akina mama na vijana, na ndiyo maana katika Kikao cha Bunge kilichopita nilisema kwamba kipindi kilichopita own source peke yake ambazo hazikupelekwa kwa kina mama na vijana zaidi ya shilingi bilioni 39; maana yake ni kwamba Madiwani na sisi tulivyokuwa katika Kamati ya Fedha hatukutimiza wajibu…
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, tafadhali naomba ufupishe majibu, tafadhali! (Makofi/Kicheko)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nilitaka angalau kidogo tuelezane hili, suala la asilimia kumi halitoki, nilikuwa nakuja asilimia kumi kutoka maana yake ni maamuzi ya wenyewe Wabunge na Madiwani, ndiyo tunakaa katika Kamati ya Fedha tunapanga kwamba asilimia kumi zitoke. Ina maana sisi tukishindwa kutimiza wajibu wetu, zitakuwa bado haziwafikii vijana, kwa sababu ten percent inafanywa katika Kamati ya Fedha ya Halmashauri husika.

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Asilimia kumi ya bajeti ya Halmashauri nchini hutengwa kwa ajili ya mikopo ya vijana na wanawake. Je, Serikali ina mkakati gani wa kusimamia fedha hizo zitolewe kwa kila Halmashauri?

Supplementary Question 2

MHE. SUKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ifahamike kwamba pesa hizi zinatengwa kwa ajili ya kusaidia vikundi vya wanawake na vijana na hasa wale wanaojiunga kupitia makundi mbalimbali. Kwa bahati nzuri nimekuwa Diwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru vipindi vinne. Pesa hizi hata kama zikitengwa katika Halmashauri nyingi nchini, kunapojitokeza jambo la dharura kwenye Halmashauri, pesa hizi zimekuwa zikitumika.
Mheshimiwa Naibu Spika, niiombe sasa Serikali itoe tamko kupitia Halmashauri zetu nchini, kunapojitokeza Halmashauri imekiuka utaratibu wa kutekeleza pesa hizi kuwafikia akina mama ni hatu gani sasa zitachukuliwa kwa Halmashauri ambazo zitashindwa kutekeleza? Ahsante

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, mimi naomba kiufupi tu niseme ifuatavyo; sasa hivi ni marufuku kwa Halmashauri yoyote asilimia kumi iliyotengwa kutowafikia vijana na kina mama na ninasema hivi sitanii.
Katika bajeti ya mwaka huu kila Halmashauri imepitishwa bajeti yake mara baada ya kutenga ile asilimia kumi; kwa hiyo Mkurugenzi yeyote na Kamati ya Fedha watakaposhindwa kutimiza wajibu huu wa Serikali, tutahakikisha Halmashauri yao tutaiwajibisha kwa sababu imeshindwa kutimiza matakwa halisi ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo tumepitisha katika bajeti ya mwaka huu wa fedha.

Name

Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Asilimia kumi ya bajeti ya Halmashauri nchini hutengwa kwa ajili ya mikopo ya vijana na wanawake. Je, Serikali ina mkakati gani wa kusimamia fedha hizo zitolewe kwa kila Halmashauri?

Supplementary Question 3

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na mazingira ya baadhi ya Halmashauri kuwa upya na changa kama ilivyo Halmashauri ya Mji wa Kondoa, vyanzo vya mapato ya ndani, huwa ni vidogo sana na hafifu; je, Serikali haioni umuhimu kupitia Wizara zake husika zenye dhamana kwa vijana na akina mama kuweka walau ruzuku fulani kufikia ukomo ili iweze kukidhi mahitaji ya vijana na akina mama?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali tumesema kwanza hii asilimia kumi siyo peke yake ndiyo inayowagusa vijana, katika Ofisi ya Waziri Mkuu, kuna Mfuko wa Uwezeshaji wa Vijana, kwa hiyo, tunachokifanya na lengo mi kwamba vijana na kina mama weweze kupata fursa kutoka maeneo mbalimbali, ninajua Halmashauri nyingine ni changa kama ulivyosema Mheshimiwa kwenye Wilaya yako ya Kondoa, Serikali imejipanga ukiacha own souce ya ten percent, kuna Mfuko wa Vijana kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, hali kadhalika kwa mujibu wa Serikali ya Chama cha Mapinduzi, katika Ilani yake imezungumza kwamba kutakuwa na mgao wa shilingi milioni 50, lengo kubwa ni kwenda kusukuma nguvu zile za vijana na kina mama katika maeneo mbalimbali kwa ajili ya shughuli za uchumi.
Kwa hiyo, nadhani kwamba mpango wa Serikali utaendelea kuboresha ili vijana na akina mama waweze kupata nguvu za kujenga uchumi katika nchi yao.

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Asilimia kumi ya bajeti ya Halmashauri nchini hutengwa kwa ajili ya mikopo ya vijana na wanawake. Je, Serikali ina mkakati gani wa kusimamia fedha hizo zitolewe kwa kila Halmashauri?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali moja tu dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ninaipongeza sana Serikali kwa kutenga asilimia kumi kwa ajili ya wanawake na vijana. Serikali sasa hivi haioni kwamba kuna umuhimu kuhakikisha inawashirikisha Wabunge wa Viti Maalum katika Halmashauri zetu, kwa kuzingatia kwamba mara nyingi pesa hizi haziwafikii walengwa. Washirikishwe kisheria na ikiwezekana washirikiane na Maofisa Maendeleo wa Miji pamoja na Kamati ya Fedha, naomba Serikali itoe tamko. Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani tukifanya reference wiki hii nilijibu swali hili siku ya Jumatatu, ushiriki wa Wabunge wa Viti Maalum katika Kamati ya Fedha, na nilizungumza kwa upana kwa ku-qoute sheria na vifungu vya kanuni. Nilitoa mifano mbalimbali katika maeneo hayo nikasema wadau watakaa wataona kama inafaa basi tuboreshe sheria zetu na kanuni zetu, hili jambo nililiongelea juzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine kwa sababu nimejua kwamba Mheshimwa Waziri wangu wa Afya alitaka ku-top up katika eneo hilo nadhani aongezee katika kipande hicho.

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Nataka tu kuongeza majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba sambamba na Halmashauri kutakiwa kutenga asilimia tano kwa ajili ya Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake; Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, imetenga shilingi bilioni moja katika bajeti ya 2016/2017 kwa ajili pia ya kuwakopesha wanawake. Kwa hiyo, fedha hizi tutazipeleka katika zile Halmashauri ambazo kwanza zimefanya vizuri, kwa hiyo kigezo ni Halmashauri kutenga za kwako, halafu Wizara yangu itaongeza zaidi ya zile ambazo zimetengwa na Halmashauri.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo, kupitia Benki ya Wanawake Wizara pia imetenga shilingi milioni 900 ambazo tutazikopesha kwa wanawake wajasiriamali katika Halmashauri mbalimbali nchini