Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CATHERINE V. MAGIGE (K.n.y. MHE. JOSEPH O. MBILINYI) aliuliza:- Je, ni lini jengo la maabara ya mionzi linalojengwa kwa muda mrefu sasa kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mbeya litakamilika na vipimo vya CT-Scan na MRI-Scan vitaletwa na kuanza kazi?

Supplementary Question 1

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, lakini tatizo lililoko Hospitali ya Rufaa ya Mbeya ni dogo sana ukilinganisha na tatizo kubwa sana lililoko katika Hospitali ya Mkoa wangu wa Arusha, Hospitali ya Mount Meru. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali ya Mount Meru hatuna CT-Scan, hatuna MRI Machine, hatuna X-Ray Processor na Ultrasound with Doppler. Kwa hiyo, wananchi wa Mkoa wa Arusha wamekuwa wakitaabika sana kwa sababu Hospitali ya Mount Meru ndiyo hospitali yetu tegemezi. Je, Serikali ina mpango gani wa kushughulikia tatizo hili katika Hoapitali ya Mount Meru haraka iwezekanavyo?

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niseme, tuna mradi wa kuboresha huduma za kiuchunguzi katika Hospitali zetu zote za rufaa za kanda na hospitali za rufaa za mikoa. Kwa hiyo, katika bajeti yangu ya 2016/2017 tumetenga kiasi cha takriban shilingi bilioni 9 kwa ajili ya kununua vifaa hivyo na kati ya hospitali ambazo tutazipa kwa mfano kama CT-Scan ni pamoja na Hospitali ya Rufaa ya Mount Meru - Arusha.
Mheshimiwa Naibu Spika, niweke wazi, vifaa kama X-Rays ni kwamba hospitali zenyewe nazo zina wajibu wa kununua vifaa tiba na sasa hivi wanaweza wakatumia Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kuomba mkopo na kununua vile vifaa tiba ambavyo gharama yake siyo kubwa. Vifaa kama CT-Scan na MRI tutaweza kuwapatia kwa kupitia mradi wa Orion.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CATHERINE V. MAGIGE (K.n.y. MHE. JOSEPH O. MBILINYI) aliuliza:- Je, ni lini jengo la maabara ya mionzi linalojengwa kwa muda mrefu sasa kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mbeya litakamilika na vipimo vya CT-Scan na MRI-Scan vitaletwa na kuanza kazi?

Supplementary Question 2

MHE. AYSHAROSE N. MATEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona na kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Tatizo la Hospitali ya Rufaa ya Mbeya ni sawasawa na matatizo yanayoikabili Hospitali ya Rufaa ya Singida. Je, Serikali ina mpango gani wa kuiboresha Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida ikiwa ni pamoja na kuipatia watumishi wa kutosha, vifaa tiba kama X-Ray na kufanya ukarabati mkubwa wa majengo ya hospitali hiyo? Ahsante.

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, ili pia kutowasimamisha Waheshimiwa Wabunge wengine, kupitia Mradi wa Orion kama nilivyosema tumetenga shilingi bilioni 9 kwa ajili ya kununua vifaa tiba, hasa vifaa vya uchunguzi katika Hospitali za Rufaa ikiwemo Sekou Toure na Singida Regional Referal Hospital, Iringa Regional Referal Hospital na Musoma Regional Referal Hospital. Kwa hiyo, naomba Waheshimiwa hawa wanaotoka katika mikoa hii wasisimame. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili kwamba ni lini sasa tutaweza kupeleka watumishi wa kutosha, kama nilivyosema tumeomba kibali cha kuajiri watumishi 30,000 katika sekta ya afya na tumeruhusiwa kuajiri watumishi 10,000. Kwa hiyo, mara taratibu zitakapokamilika, basi tutaweza pia kupeleka Madaktari Bingwa na watumishi wengine wa sekta ya afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida.

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. CATHERINE V. MAGIGE (K.n.y. MHE. JOSEPH O. MBILINYI) aliuliza:- Je, ni lini jengo la maabara ya mionzi linalojengwa kwa muda mrefu sasa kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mbeya litakamilika na vipimo vya CT-Scan na MRI-Scan vitaletwa na kuanza kazi?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja dogo la nyongeza. Nikija katika swali la msingi ambalo limeulizwa na Mbunge wa Mbeya Mjini ambalo mimi nimeletewa majibu yake hapa, naomba kuuliza swali dogo moja tu la nyongeza kwa sababu sikuuliza swali la msingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake ya matumaini ambayo ametupatia sisi Wana-Mbeya kwamba mwakani suala hili litakuwa limekamilika katika suala la msingi la Mbunge wa Mbeya Mjini. Nilitaka kujua tu Hospitali hii ya Rufaa ya Mbeya kwa sababu ndiyo inayohudumia Ukanda mzima wa Nyanda za Juu Kusini, congestion ya wagonjwa ni kubwa sana, Serikali ina mkakati gani katika kuongeza majengo ili kupata bed capacity? Ahsante.

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Dkt. Mary Mwanjelwa kwa kupigania maendeleo ya Mkoa wa Mbeya na maendeleo ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini. Nimetembelea Mbeya na nimemwona Mheshimiwa Dkt. Mary akishiriki katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo, za afya, elimu na za kuwawezesha wanawake kiuchumi. Nakupongeza sana kwa hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nikijibu swali lake, ni kweli Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Mbeya inahudumia mikoa takriban minne; Mikoa ya Mbeya, Songwe, Njombe, Iringa, Ruvuma, Rukwa na Katavi. Kwa hiyo, kwetu sisi ni hospitali ambayo tunaipa kipaumbele cha kutosha. Katika kumthibitishia hili, tunafanya mipango ya kuongeza kujenga jengo kwa ajili ya kuhudumia wanawake wajawazito katika kile Kitengo cha Hospitali ya Wanawake cha Meta.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tutaanza kwanza kuongeza jengo kwa ajili ya akina mama wajawazito halafu tutapanua miundombinu, tunataka pia Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Mbeya itoe huduma pia ya matibabu ya saratani badala ya wananchi kuhangaika kwenda Dar es Salaam. Tunataka huduma kama hizo za saratani pia ziweze kupatikana na Hospitali ya Rufaa ya Mbeya.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kumthibitishia Mheshimiwa Dkt. Mary Mwanjelwa, kwa sababu makusanyo ya Serikali ya Awamu ya Tano ni makubwa sana, tuna matumaini kwamba tutapata hela kama tulivyoweka katika bajeti yetu ili tuweze kutekeleza mipango hiyo ya miradi ya maendeleo ambayo tumeipanga.