Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH (K.n.y. MHE. HASSAN S. KAUNJE) aliuliza:- Kuna migogoro ya ardhi iliyosababishwa na upimaji na ugawaji wa ardhi kwa ajili ya makazi na ujenzi wa taasisi katika Kata ya Rasbura eneo la Mitwero. Aidha, watumishi wa Idara ya Ardhi walijigawia ardhi kinyume na taratibu na kuiuza kwa manufaa yao. Pia wananchi wanalalamikia fidia na utwaaji wa maeneo makubwa tofauti na michoro iliyomo kwenye nyaraka zilizothibitishwa na Wizara kwa matumizi ya taasisi za umma au binafsi:- Je, Serikali ipo tayari kufanya uchunguzi au uhakiki wa zoezi zima la upimaji na ugawaji wa viwanja katika eneo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, namshuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Hata hivyo, bado watu wa Kata ya Rasbura Kijiji cha Mitwero wanaendelea kulalamikia kuhusu tatizo hili ambalo lipo. Fidia ambazo wamelipwa wananchi wale ni ndogo kiasi kwamba wanashindwa kununua maeneo mengine mbadala ili waendelee kufanya shughuli zao. Je, Serikali itawasaidiaje wananchi hawa kupata maeneo mengine mbadala ili waendelee kufanya shughuli zao?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, katika jibu langu la msingi nimesema kwamba Wizara yangu ikishirikiana pia na Ofisi ya Manispaa ya kule, kuna utaratibu uliokuwa unafanywa wa kupitia upya maeneo yale ili kuweza kuona wale ambao wamelipwa fidia ndogo kulingana na thamani ya ardhi ambayo imetwaliwa wanapata stahiki zao. Ndiyo maana nimesema zoezi hili lilikuwa linafanyika upya. Mpaka wakati huu napozungumza, baadhi ya taasisi ambazo zilikuwa zimechukua maeneo hayo zimekwishawalipa watu hao fidia zao na wanaendelea na taratibu zao za kawaida.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, suala la kusema kwamba tutawasaidiaje kupata maeneo, unapotoa ardhi yako kwa mtu au taasisi kinachotakiwa kulipwa ni ile fidia stahiki ambayo itakufanya wewe pia uweze kupata eneo lingine la kuanzisha makazi mengine au maendeleo mengine kwa kadri ambavyo utakuwa umejipanga. Kwa sababu fidia yoyote inayochukuliwa lazima iende na bei ya soko. Tatizo tulilonalo, baadhi ya wananchi wanakuwa na ule uharaka wa kutoa ardhi yao na wanapewa fidia ndogo ambayo haiwezi kuwafikisha mahali ambapo wanastahili.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kupitia Bunge hili tunasema kwamba ni marufuku kwa watu kuwanyanyasa wananchi kwa kuwapa fidia ndogo ambazo hazikidhi mahitaji. Ndiyo maana vilevile tumesema kuanzia sasa hakuna ardhi itakayotwaliwa bila Wizara yangu kujiridhisha na fidia ambayo itakuwa imetathminiwa kwa wale ambao ardhi yao inakwenda kutwaliwa, ni lazima fidia ifuate bei ya soko itakayokuwepo kwa wakati huo.

Name

Sixtus Raphael Mapunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH (K.n.y. MHE. HASSAN S. KAUNJE) aliuliza:- Kuna migogoro ya ardhi iliyosababishwa na upimaji na ugawaji wa ardhi kwa ajili ya makazi na ujenzi wa taasisi katika Kata ya Rasbura eneo la Mitwero. Aidha, watumishi wa Idara ya Ardhi walijigawia ardhi kinyume na taratibu na kuiuza kwa manufaa yao. Pia wananchi wanalalamikia fidia na utwaaji wa maeneo makubwa tofauti na michoro iliyomo kwenye nyaraka zilizothibitishwa na Wizara kwa matumizi ya taasisi za umma au binafsi:- Je, Serikali ipo tayari kufanya uchunguzi au uhakiki wa zoezi zima la upimaji na ugawaji wa viwanja katika eneo hilo?

Supplementary Question 2

MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa tatizo la Kata ya Rasbura linafanana na tatizo lililoko Kata la Lusonga Jimbo la Mbinga Mjini ambapo Halmashauri ilitwaa eneo ambalo lilikuwa linamilikiwa na wananchi kwa malengo ya kupima viwanja na kuliboresha eneo lile lakini mpaka sasa fidia bado haijalipwa na viwanja bado vinaendelea kugawanywa kwa watu wengine. Serikali haioni sasa hiyo formula inayotumika kule Lindi ikatumike na Mbinga yaani kulirudia tena kulipima upya na wale wananchi wa Lusonga wapate haki yao?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, wazo lake ni zuri, nami nalikubali kama Wizara. Kikubwa ambacho nataka kusema ni kwamba, kabla ya utoaji wa ardhi katika maeneo yoyote, tuwaombe sana Halmashauri zinazohusika lazima wahusishe Ofisi ya Mthamini Mkuu ili waweze kuona kwamba tathmini itakayofanyika haimpunji mtu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwa sababu anasema kule kwake kuna tatizo, namwomba sana, kwa sababu hatujapata kwa maandishi kwamba kuna matatizo hayo, ashirikiane na Kanda yetu ya Ardhi kule kwa maana ya Kamishna ili waweze kuliangalia suala hili. Kama kuna malalamiko ambayo yapo, basi ofisi itakuwa tayari kuyasikiliza na kuweza kuipitia upya. Kwa sababu hatujalipokea, siwezi kulitolea jibu la moja kwa moja, isipokuwa ni kushirikiana na Kamishna wa Kanda katika Kanda ambayo Mheshimiwa anatoka.

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH (K.n.y. MHE. HASSAN S. KAUNJE) aliuliza:- Kuna migogoro ya ardhi iliyosababishwa na upimaji na ugawaji wa ardhi kwa ajili ya makazi na ujenzi wa taasisi katika Kata ya Rasbura eneo la Mitwero. Aidha, watumishi wa Idara ya Ardhi walijigawia ardhi kinyume na taratibu na kuiuza kwa manufaa yao. Pia wananchi wanalalamikia fidia na utwaaji wa maeneo makubwa tofauti na michoro iliyomo kwenye nyaraka zilizothibitishwa na Wizara kwa matumizi ya taasisi za umma au binafsi:- Je, Serikali ipo tayari kufanya uchunguzi au uhakiki wa zoezi zima la upimaji na ugawaji wa viwanja katika eneo hilo?

Supplementary Question 3

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Mwaka 2011/2012 Bunge hili liliazimia kuanzisha Mabaraza ya Ardhi matano. Miongoni mwa Mabaraza hayo ni pamoja na Wilaya ya Tunduru kuanzisha Baraza la Ardhi lakini mpaka sasa hivi tunavyozungumza Wilaya ya Tunduru katika Baraza lile la Ardhi bado halina Mwenyekiti, Mwenyekiti ni lazima atoke Songea aje Wilayani Tunduru. Ni lini sasa Serikali itachukua hatua ya kuona kuwa tunapata Mwenyekiti ambaye atakuwa anashughulikia migogoro ya ardhi iliyopo Wilayani Tunduru? Ahsante.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza swali lake liko nje na lile swali la msingi lakini kwa sababu ameuliza naomba tu nitolee maelezo.
Mheshimiwa Naibu Spika, wakati wa bajeti ya Wizara tulitoa orodha ya Halmashauri zote au Wilaya zote ambazo Mabaraza mapya yanakwenda kuanzishwa na yalikuwa ni Mabaraza 47 ambayo yamepangwa, lakini kwa kuanzia tukasema ni Mabaraza matano. Kesi yake katika Jimbo lake analolisema tunaitambua lakini kulingana na ule ufinyu wa bajeti iliyopo tumeshindwa kuwa na Wenyeviti wa kutosheleza Mabaraza hayo ambayo tutakwenda kuanzia nayo. Ndiyo maana tulisema tumeomba ombi maalumu kwenye Wizara ya Utumishi ili kutupa kibali tuweze kupata Wenyeviti tuwasambaze katika maeneo yote ambayo hayana Mabaraza na ambako kuna matatizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Kwa hiyo, pale ambapo tutapewa kibali hicho, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwenye Baraza analolizungumzia ambalo halina Mwenyekiti kwenye Jimbo lake basi tutampatia. Kwa sasa bado tunasubiri kibali kutoka Wizara ya Utumishi.

Name

Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH (K.n.y. MHE. HASSAN S. KAUNJE) aliuliza:- Kuna migogoro ya ardhi iliyosababishwa na upimaji na ugawaji wa ardhi kwa ajili ya makazi na ujenzi wa taasisi katika Kata ya Rasbura eneo la Mitwero. Aidha, watumishi wa Idara ya Ardhi walijigawia ardhi kinyume na taratibu na kuiuza kwa manufaa yao. Pia wananchi wanalalamikia fidia na utwaaji wa maeneo makubwa tofauti na michoro iliyomo kwenye nyaraka zilizothibitishwa na Wizara kwa matumizi ya taasisi za umma au binafsi:- Je, Serikali ipo tayari kufanya uchunguzi au uhakiki wa zoezi zima la upimaji na ugawaji wa viwanja katika eneo hilo?

Supplementary Question 4

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Miji ya Sumve, Nyamatala, Malya, Nyambiti, Hungumarwa inakua kwa kasi sana. Mheshimiwa Waziri katika ziara yake aliyoifanya Kwimba nilimuomba vitendea kazi kama gari na vifaa vya kupimia. Nataka kujua ombi letu hilo limefikia wapi?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nilitembelea kwenye Jimbo lake na hayo anayoyasema tuliyazungumza. Kikubwa ambacho nataka nimhakikishie, katika bajeti yetu ambayo imepitishwa na hata kwenye bajeti ya Wizara ya Fedha ambayo tunaendelea kuijadili, kuna fedha kiasi cha shilingi bilioni 8.8 zimetengwa kwa ajili ya kununua vifaa vya upimaji kwa sababu tatizo la upimaji ni tatizo kubwa katika nchi yetu na tunasema eneo lililopimiwa ni asilimia 15 tu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, pale ambapo tutakuwa tumefanikiwa kupata pesa hizo baada ya kuwa tumepitisha bajeti hii tunajua hizo shilingi bilioni 8.8 kwa ajili ya kununua vifaa vya upimaji ziko pale. Tukishapata, vifaa hivyo vitakwenda katika Kanda. Jimbo la Sumve liko kwenye Kanda ya Ziwa, kwa maana hiyo, eneo la Kanda wakipata vifaa hivyo basi upimaji katika maeneo ya Nyamatala na mengine aliyoyasema yatafanyiwa upimaji kwa wakati muda utakapofika.