Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:- Malambo ya Kijiji cha Mikomahiro, Salamakati, Salama „A‟, Sanzati, Mgeta, Kihumu/Hunyari na Nyang‟aranga yamekuwa hayatumiki ipasavyo kutokana na magugu maji na hivyo kujaa matope:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha malambo haya ili yatoe huduma nzuri kwa watumiaji? (b) Malambo haya yalichimbwa miaka ya nyuma na watumiaji kwa sasa wameongezeka; je, Serikali ina mpango wa kuyapanua malambo hayo ili kukidhi mahitaji ya watumiaji kwa sasa?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba tu kutoa ufafanuzi tena kwamba Wilaya ya Bunda ina Majimbo matatu. Kuna Mwibara ya Mheshimiwa Kangi Lugola; kuna Bunda Mjini kwa Mheshimiwa Ester Bulaya na kuna Jimbo la Bunda kwa Mheshimiwa Boniphace Mwita Getere. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Namshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri lakini naomba Mawaziri au Manaibu Waziri wanapokuwa wanapata hayo majibu kutoka kwenye Halmashauri wawe wanayatazama vizuri kwa sababu majibu ninayoyaona hapa yanahusu mpango wa Halmashauri siyo swali la Boniphace Mwita kwenye Jimbo la Bunda.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mimi nimeuliza mambo ya malambo unaniambia kuna gharama za kujenga mnada, sasa hainiletei faida kwenye swali langu hili. Naomba kujua tu, ni lini hizi shilingi milioni 90, shilingi milioni 200 na shilingi milioni 110 ambazo Naibu Waziri amezitaja kwamba zitatumika kukarabati na kujenga malambo hayo zitapelekwa Bunda na zitatoka chanzo gani?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, naomba kujua, malambo hayo sita ya kukarabati ambayo Naibu Waziri ameyataja hapa na matano ya kujengwa, yatajengwa vijiji gani? Maana naona kama hii ni jumla ya Wilaya ya Bunda yote.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, suala kwamba lini pesa hizo zitapelekwa ni kama nilivyosema katika jibu langu la msingi. Mheshimiwa Getere pia lazima akubali kwamba kama alivyosema awali kwamba Bunda ina Majimbo matatu, Bunda la Mjini, halikadhalika na Jimbo la Mwibara la kaka yangu pale Mheshimiwa Kangi Lugola, mipango yote ya fedha maana yake ninyi mnapokaa katika Halmashauri yenu ndiyo mnafanya maamuzi sasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, haiwezekani Jimbo likatengeneza bajeti yake kama Jimbo isipokuwa kama Halmashauri ambayo ina Majimbo matatu ndiyo inapanga hivyo vipaumbele. Ndiyo maana katika jibu langu la msingi nimeainisha jinsi gani mlipanga mipango ya miaka mitatu katika ukarabati na ujenzi wa yale malambo mengine matano. Kwa hiyo, lini fedha hizo zitakwenda, ndiyo maana nimesema katika mwaka huu wa fedha mlianza kutenga bajeti ambayo kuanzia Julai ndiyo mwaka wa fedha huwa unaanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika eneo la pili kuweza kusema vijiji specific, Mheshimiwa Mbunge naomba niweze kusema wazi kwamba kwa hapa itakuwa vigumu kwa sababu Halmashauri imepanga mpango wake huu na kuainisha vijiji, nadhani tuwasiliane baadaye tuone jinsi gani tutafanya. Vilevile tuangalie na ninyi kule katika Halmashauri mpango mlioupanga mlisema mtatekeleza mradi huu katika vijiji gani.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie kwamba kilio cha Wanajimbo lake la Bunda kimesikika. Jukumu letu kubwa ni kuhakikisha sasa Wanabunda katika Jimbo lake wanapata mahitaji yale ambayo wanayakusudia. Mwisho wa siku kama wananchi wa kawaida au kama wafugaji wa kawaida basi waweze kupata maji kwa ajili ya malisho yao na matumizi mengine ya nyumbani.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:- Malambo ya Kijiji cha Mikomahiro, Salamakati, Salama „A‟, Sanzati, Mgeta, Kihumu/Hunyari na Nyang‟aranga yamekuwa hayatumiki ipasavyo kutokana na magugu maji na hivyo kujaa matope:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha malambo haya ili yatoe huduma nzuri kwa watumiaji? (b) Malambo haya yalichimbwa miaka ya nyuma na watumiaji kwa sasa wameongezeka; je, Serikali ina mpango wa kuyapanua malambo hayo ili kukidhi mahitaji ya watumiaji kwa sasa?

Supplementary Question 2

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa muda wa kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Serikali imefanya feasibility study (upembuzi yakinifu) kwenye malambo mengi na kwa kuwa swali la msingi la Bunda linafanana na Mbulu Vijijini na Mbulu Mjini, je, Serikali ina mpango gani kuyajenga malambo hayo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli huwezi kufanya jambo lolote katika mradi mkubwa bila kufanya upembuzi kwanza kuangalia jinsi utakavyotekeleza mradi huo. Kama alivyosema katika eneo lake kuna maeneo ambayo wamefanya feasibility study kujua gharama ya ujenzi itakuwaje na anataka kujua ni lini sasa kazi hii itafanyika. Naomba niseme wazi kwamba katika mchakato huu wa bajeti kila Halmashauri imetengewa bajeti yake kutokana na vipaumbele vilivyowekwa na bahati mbaya tulikuwa na ukomo wa bajeti.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, inawezekana feasibility study imeshafanyika lakini mradi haujionyeshi katika mwaka huu wa fedha. Lengo kubwa ni ndani ya kipindi cha miaka mitano mradi ule uweze kutekelezwa. Imani yangu kubwa ni kwamba kama feasibility study imefanyika, kama fedha hiyo haijatengwa specific katika Jimbo lake katika mwaka huu wa fedha, basi katika mchakato wa bajeti ya mwaka unaokuja itakuwepo ili malambo yajengwe wananchi wapate huduma ya maji.

Name

Andrew John Chenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:- Malambo ya Kijiji cha Mikomahiro, Salamakati, Salama „A‟, Sanzati, Mgeta, Kihumu/Hunyari na Nyang‟aranga yamekuwa hayatumiki ipasavyo kutokana na magugu maji na hivyo kujaa matope:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha malambo haya ili yatoe huduma nzuri kwa watumiaji? (b) Malambo haya yalichimbwa miaka ya nyuma na watumiaji kwa sasa wameongezeka; je, Serikali ina mpango wa kuyapanua malambo hayo ili kukidhi mahitaji ya watumiaji kwa sasa?

Supplementary Question 3

MHE. ANDREW J. CHENGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Napenda niiulize Serikali, kwa sababu tatizo hili ni kubwa katika maeneo mengi nchini na nichukue tu kwa upande wa Jimbo langu la Bariadi na Jimbo la jirani la Itilima, malambo kama la Sakwe, Igegu, Sapiwi, Matongo, Mwamapalala na Mwamoto yote haya yameshambuliwa na magugu maji na maeneo mengi nchini najua hali ni hii.
MHE. ANDREW J. CHENGE: Na Malya. Je, Serikali haiwezi ikaja na mpango kabambe kama ilivyofanya kwa Ziwa Victoria miaka ya 1990 wakati limeshambuliwa na magugu maji ili kunusuru malambo haya hasa katika maeneo ambayo tuna pressure kubwa sana ya population kuliko kuziachia Halmashauri kwa mtindo huu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Chenge amezungumzia suala la mpango kabambe wa kushughulikia tatizo la magugu maji lakini kuhakikisha kwamba huduma ya maji inapatikana kwa wananchi. Nadhani Waziri wa Maji katika bajeti yake alizungumzia suala la kukamilika kwa mpango wa maji wa awamu ya kwanza sasa tunaendelea katika mpango wa maji wa awamu ya pili.
Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa maji wa awamu ya pili maelekezo yake ni nini? Maelekezo yake ni kwamba tutabainisha fursa mbalimbali, kwa mfano, ukiacha watu wa Kanda ya Ziwa wanaopata fursa ya maji kutoka Ziwa Victoria lakini na maeneo mbalimbali kuona ni jinsi gani wataweza kupata maji. Ndiyo maana nikimkumbuka au nikim-quote Waziri wa Maji alisema tutaangalia fursa zote zilizokuwepo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna maeneo mengine yamechimbwa visima virefu (bore holes) lakini vimekosa maji. Ndiyo maana ya maelekezo haya kwamba kila Halmashauri angalau kwa mwaka mmoja itenge fedha kwa ajili ya ujenzi wa lambo moja. Huo ni mpango mdogo wakati mpango mkubwa ni kwamba katika miaka hii mitano inayokuja ya ya programu ya maji ya kuhakikisha tunamtua ndoo mama kichwani tutahakikisha tunatumia fursa mbalimbali ikiwemo mito mikubwa, malambo na hata maziwa ya jirani ili mradi wananchi wa maeneo husika wapate maji. Kwa hiyo, napenda kumjulisha Mheshimiwa Chenge kamba jambo lake Serikali imelisikia na ndiyo mkakati mpana wa Serikali katika kuhakikisha tunamtua ndoo mama kichwani kama tulivyoahidi katika Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi.

Name

Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:- Malambo ya Kijiji cha Mikomahiro, Salamakati, Salama „A‟, Sanzati, Mgeta, Kihumu/Hunyari na Nyang‟aranga yamekuwa hayatumiki ipasavyo kutokana na magugu maji na hivyo kujaa matope:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha malambo haya ili yatoe huduma nzuri kwa watumiaji? (b) Malambo haya yalichimbwa miaka ya nyuma na watumiaji kwa sasa wameongezeka; je, Serikali ina mpango wa kuyapanua malambo hayo ili kukidhi mahitaji ya watumiaji kwa sasa?

Supplementary Question 4

MHE. KANGI A. N. LUGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa fursa kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa mwaka 2015 niliuliza hapa Serikali imejipanga vipi kupambana na magugu maji kwenye lambo la Kabainja ambalo liko Wilaya ya Bunda Jimbo la Mwibala na Serikali hii ikaahidi Bunge hili kwamba malambo yote ambayo yana magugu maji na malambo yote ambayo yalichakachuliwa kwa maana kwamba hayakukamilika itatenga fedha na kuanzisha mpango maalum ambao nadhani Mheshimiwa Chenge alikuwa anashauri. Je, kwa nini Serikali sasa haizungumzii mpango huu ambao waliuzungumzia mwaka 2015 sasa wanaanza kutupa majibu mengine mapya kana kwamba ndiyo wanataka wajipange upya? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, haya siyo majibu mapya ni mpango ule ule wa Serikali unaendelea. Nimjulishe Mheshimiwa Kangi Lugola lengo letu ni nini. Maana suala la magugu maji ni jambo moja lakini malambo mengine tukiyafanyia utafiti kuna mengine yanakufa kutokana na shughuli za kijamii ambazo zinazunguka malambo hayo. Kwa hiyo, mpango wa Serikali katika kuhakikisha tunapambana na magugu maji uko pale pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, sitaenda kwenye detail ya kila Halmashauri kuonyesha imejipanga vipi katika kushughulikia suala hilo lakini tunaendelea vilevile na suala la kutoa elimu maana kuna maeneo ambapo malambo yanakufa siyo kwa sababu ya magugu maji bali ni kutokakana na kazi za kijamii hasa kilimo. Watu wanapofanya shughuli za kilimo na mifugo kuzunguka haya malambo mwisho mvua inaponyesha udongo unasombwa unajaza malambo na kusababisha yafe.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tuna mpango mpana, licha ya suala la magugu maji lakini elimu katika maeneo mbalimbali inaendelea kutolewa kwa wananchi. Lengo kubwa ni kuhifadhi vyanzo vya maji ili visije vikafa kabla ya muda uliokadiriwa. Hili limekuwa ni tatizo kubwa hasa malambo mengi kujaa matope na mchanga ukiachia magugu maji ambapo ndani ya muda mfupi yanakufa lakini inasababishwa na wakazi wenyewe wa maeneo haya.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kama Serikali tumeendelea kutoa elimu na tunaomba sana ushirikiano wa Waheshimiwa Wabunge wote. Agenda hii ni yetu sote, lazima tupambane nayo. Mwisho wa siku ni kuhakikisha kila mwananchi anapata maji katika maeneo yake.