Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 45 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 387 2016-06-17

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:-
Je, ni aina gani ya madini yanapatikana ndani ya Wilaya ya Kalambo kulingana na tafiti ambazo zimekwishafanywa na Serikali?
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Sinkamba Kandege, Mbunge wa Kalambo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na tafiti za awali zilizofanywa na Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST) pamoja na taarifa kutoka kwa wawekezaji wanaomiliki leseni katika maeneo ya Kalambo, madini yanayopatikana ni pamoja na madini ya chuma, dhahabu, galena kwa maana ya lead, shaba pamoja na madini ya ujenzi. Hata hivyo, GST wanaendelea kufanya utafiti katika maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na Wilaya ya Kalambo ili kubaini kama kuna madini mengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa nitumie nafasi hii kuwaomba wananchi wenye nia ya kupata taarifa kuhusu rasilimali za madini yaliyopo katika maeneo hayo, wafike katika ofisi zetu za madini pamoja na Wakala wake. Aidha, taarifa hizo zinapatikana kwenye tovuti ya Wizara, tovuti ya GST pamoja na machapisho mbalimbali ambayo yapo katika Ofisi zetu za madini.