Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 28 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 245 2022-05-23

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatoa fedha ili kukamilisha ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji katika Kata ya Ifumbo, Chunya?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Masache Njelu Kasaka, Mbunge wa Lupa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa Skimu ya Umwagiliaji ya Ifumbo yenye eneo la hekta 250 inayolima mazao ya mpunga, alizeti, ufuta, mbogamboga na mahindi kwa wananchi wa Chunya. Kwa kutambua umuhimu wa skimu hiyo, Serikali ilitenga kiasi cha shilingi milioni 400 kupitia Programu ya Kuendeleza Kilimo na shilingi milioni 50 kupitia Programu ya Kuendeleza Kilimo Wilayani katika mwaka wa fedha 2008/2009. Fedha hizo zilitumika kujenga miundombinu ya umwagiliaji ikiwemo banio, vigawa maji 11, vivuko vya miguu 10 na mfereji mkuu wenye urefu wa mita 2,165.

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kilimo cha umwagiliaji nchini na hasa ukizingatia mabadiliko ya tabia nchi yanayopelekea mtawanyo wa mvua zisizotabirika. Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kukamilisha Skimu ya Ifumbo na zingine zote za umwagiliaji nchini.