Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 28 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 243 2022-05-23

Name

Assa Nelson Makanika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Primary Question

MHE. ASSA N. MAKANIKA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi watakaoathirika na ujenzi wa barabara ya Mwandiga – Manyovu Mkoani Kigoma?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Assa Nelson Makanika, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara ya Mwandiga – Manyovu yenye urefu wa kilometa 53 ilianza kujengwa kwa kiwango cha lami mwezi Agosti, 2008 na kukamilika mwezi Oktoba, 2010. Wakati wa ujenzi wa barabara hii Wananchi wote waliostahili kulipwa fidia kwa mujibu wa sheria kutokana na mali zao kuathirika na ujenzi huo walilipwa fidia. Ahsante.