Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 28 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 240 2022-05-23

Name

Mohamed Suleiman Omar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malindi

Primary Question

MHE. MOHAMED SULEIMAN OMAR aliuliza:-

Je Serikali ina mpango gani wa kupitia upya fedha za Mfuko wa Vichocheo vya Maendeleo ya Majimbo na kuziongeza fedha kwa upande wa Zanzibar?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Suleiman Omar, Mbunge wa Jibo la Malindi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kifungu cha 5(3) cha Sheria ya Mfuko wa Jimbo kimefafanua vigezo vinavyotumika kugawa fedha za Mfuko wa Kuchochea Maendeleo ya Jimbo kama ifuatavyo:-

(a) Mgao sawa kwa kila jimbo asilimia 25;
(b) Idadi ya watu katika jimbo asilimia 45;
(c) Kiwango cha umaskini katika Jimbo 20; na
(d) Ukubwa wa eneo katika Jimbo 10.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuangalia uwezekano wa kuboresha mgao wa fedha za Zanzibar kulingana na upatikanaji wa mgao. Ahsante.