Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 45 Public Service Management Ofisi ya Rais TAMISEMI. 380 2016-06-17

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:-
Makao Makuu ya Wilaya ya Uyui yapo Isikizya eneo ambalo halina miundombinu, nyumba za kuishi na huduma rafiki kwa wafanyakazi. Shirika la Nyumba la Taifa limejenga nyumba Isikizya na lilipendekeza kuuza nyumba hizo kwa Halmashauri ya Uyui na kumaliza malipo ndani ya miaka mitatu lakini Halmashauri haina uwezo wa kumaliza malipo ndani ya miaka mitatu. Hivyo wafanyakazi wa Halmashauri wanaendelea kuishi katika nyumba za kupanga Mjini Tabora:-
(a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuchangia ununuzi wa Nyumba za Shirika la Nyumba (NHC) ili wafanyakazi wa Halmashauri ya Uyui wahamie Isikizya?
(b) Shirika la Nyumba ni wadau wa maendeleo ya makazi na kwa kuwa Serikali ina nia ya kusaidia uanzishwaji wa Makao Makuu ya Wilaya ya Uyui, je, kwa nini Serikali isishawishi Shirika la Nyumba kuongeza muda wa kuuza nyumba zake kutoka miaka mitatu hadi kumi ili kuwezesha Halmashauri kulipa polepole?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Almas Athuman Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2015/2016, Halmashauri ya Wilaya ya Tabora/Uyui ilitenga shilingi milioni 174.6 kwa ajili ya ununuzi wa nyumba tatu za watumishi ambazo zimejengwa na Shirika la Nyumba la NHC ili watumishi wa Halmashauri hiyo wahamie Isikizya yalipo Makao Makuu ya Halmashauri. Vilevile katika mwaka wa fedha 2016/2017, zimetengwa shilingi milioni 150 kutokana na mapato ya ndani kwa ajili ya ununuzi wa nyumba zaidi za watumishi.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa kifungu 14 (1) cha Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa, Sura 290, Mamlaka za Serikali za Mitaa zimepewa mamlaka ya kukopa katika taasisi mbalimbali za ndani au kuingia mikataba ya
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
8
manunuzi baada ya kupata kibali cha Waziri mwenye dhamana. Hata hivyo, katika kufanya hivyo Halmashauri zinapaswa kuzingatia uwezo uliopo katika kurejesha mkopo husika. Hivyo, Halmashauri inashauriwa kununua nyumba za NHC kwa kuzingatia uwezo uliopo katika bajeti iliyotengwa kwa mwaka 2016/2017.