Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 45 Justice and Constitutional Affairs Ofisi ya Rais TAMISEMI. 379 2016-06-17

Name

Freeman Aikaeli Mbowe

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI (K.n.y. MHE. FREEMAN A. MBOWE) aliuliza:-
Mfumo wa Vyama Vingi vya Siasa huwapa wananchi fursa ya kuchagua kiongozi na chama wanachotaka sambamba na Ilani za Vyama husika katika kila ngazi ya uchaguzi kuanzia ya Mtaa/Kijiji, Kata, Jimbo na Taifa:-
(a) Je, ni kwa nini Serikali ya CCM hupuuza ukweli huu na kulazimisha Ilani ya Chama chao kutekelezwa nchi nzima kila ngazi bila kujali matakwa ya wananchi kupitia uchaguzi?
(b) Je, katika mazingira ya Manispaa au Halmashauri za Wilaya palipo na uongozi wa Chama tofauti na CCM ni ipi mipaka ya Wakuu wa Wilaya na Mikoa kutoa amri au maelekezo ya kiutendaji?
(c) Je, Serikali haioni kuwa sasa ni wakati muafaka kuweka utaratibu wa kisheria na kikanuni ili kuondokana na mfumo huu kandamizi ambao ni urithi na ukiritimba wa mfumo wa chama kimoja cha siasa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Freeman Aikaeli Mbowe, Mbunge wa Hai, lenye sehemu (a), (b) na (c) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Ibara ya 3(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inabainisha wazi kuwa nchi yetu inafuata mfumo wa Vyama Vingi vya Siasa. Mfumo huo popote pale duniani hukipa Chama Tawala fursa na haki ya kuelekeza kutokana na ridhaa ya wananchi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, dhana hii ya vyama vingi inatumika pia katika mazingira ya Manispaa na Halmashauri. Vivyo hivyo, mipaka ya Wakuu wa Mikoa na Wilaya kutoa amri au maelekezo ya kiutendaji katika maeneo yao ya utawala, iko kwa mujibu wa Ibara ya 61(4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na vifungu vya 5 (1)-(3) na 14(1)-(3) vya Sheria ya Utawala wa Mikoa, Sura ya 97. Hivyo, Serikali inaamini kuwa utaratibu huu umezingatia demokrasia na kwa sasa hakuna umuhimu wa kuweka mfumo mwingine. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali haioni ukiritimba wowote katika mfumo uliopo, hivyo sheria na mifumo iliyopo itaendelea kufanya kazi.