Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 5 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 60 2016-02-01

Name

Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE aliuza:-
Wanachi wa Mikumi upande mmoja wamebanwa na Hifadhi na upande wa pili ardhi kubwa wamepewa Wawekezaji ambao hawajafanya uendelezaji wowote katika mashamba ya Kisanga, Masanze, Tindiga na hiyo kupelekea wananchi kukosa ardhi:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuirudisha ardhi hii kwa wananchi ili waweze kujiletea maendeleo?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Leonard Haule, Mbunge wa Mikumi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Jimbo la Mikumi ni miongoni mwa maeneo ambayo yana ardhi nzuri kwa kilimo na ambalo pia lina wakulima na wawekezaji wenye mashamba makubwa.
Mheshimiwa Spika, ili kuitwaa ardhi kwa yeyote ambaye ameshindwa kuiendeleza utaratibu ufuatao unapaswa kufuatwa:-
Mheshimiwa Spika, kwanza sheria inataka mmiliki apatiwe ilani ya ubatilisho ya siku 90 na mamlaka (Halmashauri) husika ambapo shamba lipo. Ilani hiyo inatakiwa kueleza masharti yaliyokiukwa na kwa nini miliki yake isifutwe. Vile vile muda huo unampa mmiliki muda wa kuwasilisha utetezi wake kwa mujibu wa kifungu cha 47, 48 na 49 cha Sheria ya Ardhi Na. 4 ya mwaka 1999.
Pili, muda wa ilani ya ubatilisho utakapokuwa umekwisha mapendekezo ya ubatilisho yatatumwa kwa Kamishna ambapo kama Kamishna atakubaliana na sababu za mapendekezo ya ubatilisho, Kamishna atawasilisha mapendekezo kwa Waziri mwenye dhamana ambaye naye atawasilisha mapendekezo hayo kwa Mheshimiwa Rais na kumshauri afute miliki hiyo.
Mheshimiwa Spika, naishauri Halmashauri husika ifanya ukaguzi wa mashamba yote makubwa yaliyomo ndani ili yale yaliyokiuka sheria hatua zinazofuata zichukuliwe.