Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 51 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 677 2023-06-20

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza:-

Je, ni kwa namna gani Serikali inalinda afya ya mama mjamzito na mtoto mchanga?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Husna Juma Sekiboko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kulinda afya ya mama mjamzito na mtoto mchanga, Wizara inafanya yafuatayo:-

(1) Kila mama mjamzito anayehudhuria kliniki anapata vipimo muhimu ikiwemo vipimo vya wingi wa damu, shinikizo la damu na kipimo cha protini kwenye mkojo ili kubaini mapema matatizo ya ujauzito;

(2) Matibabu na huduma ya mama mjamzito na watoto chini ya miaka mitano yanatolewa bila malipo katika vituo vyote vya Serikali;

(3) Serikali imeimarisha upatikanaji wa vifaa tiba kwa ajili ya kutibu matatizo yatokanayo na uzazi kwa kufikia asilimia 50 kwa vituo vyote vya kutolea huduma; na

(4) Watoa huduma za afya ya uzazi wamejengewa uwezo ili waweze kutoa huduma stahiki kwa akina mama wanaopata changamoto za uzazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe rai kwa wananchi wote hasa akina mama wajawazito kuhakikisha wanahudhuria kliniki na pia kujifungulia katika vituo vya kutolea huduma, ahsante.