Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 51 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 676 2023-06-20

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa dawa zinapatikana wakati wote katika hospitali, vituo vya afya na zahanati nchini?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asia Abdukarimu Halamga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhakikisha dawa zinapatikana wakati wote kwenye vituo vya kutolea huduma za afya, Serikali inatekeleza na kusimamia yafuatayo:-

i. Kuiwezesha MSD mtaji ili iweze kufanya kazi kama bohari ya dawa badala ya kufanya kazi kama idara ya manunuzi,

ii. Utoaji wa fedha za kununua, kutunza na kusambaza dawa kila mwezi kiasi cha shilingi bilioni 16,

iii. Kuboresha utendaji wa MSD na kuiwezesha kuwa na mikataba ya muda mrefu ya ununuzi wa dawa,

iv. Kuboresha maoteo ya bidhaa za afya na kuchukua hatua kwa upungufu unaobainika,

v. Kufunga mifumo ya kielektroniki ili kuimarisha usimamizi wa dawa na kuwezesha dawa kutolewa kulingana na wagonjwa husika,

vi. Kusimamia Muongozo wa matibabu katika kuhakikisha dawa zinazonunuliwa, kutunzwa na kuandikwa na Madaktari zinazingatia muongozo wa matibabu,

vii. Kudhibiti mianya ya upotevu na wizi kwa kuwa na kaguzi za mara kwa mara ili kuhakikisha dawa zinakuwepo vituoni,

viii. Kuanzisha maduka ya dawa ya hospitali za umma yatakayokuwa na dawa muda wote kwa ajili ya wagonjwa wa ndani na nje ya hospitali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kuzielekeza Halmashauri na viongozi wote wa vituo vya kutolea huduma za afya kuhakikisha wanatumia zaidi ya asilimia 50 ya mapato yao kununua dawa na bidhaa nyinginezo za afya.