Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 51 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 675 2023-06-20

Name

Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU K.n.y. MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itajenga majosho katika Kata za Kolo, Kingale na Bolisa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Ally Juma Makoa, Mbunge wa Kondoa Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na mpango wa ujenzi wa majosho nchini ili kudhibiti magonjwa yanayoenezwa na kupe. Katika mwaka wa fedha wa 2023/2024 Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Sekta ya Mifugo, imetenga jumla ya shilingi bilioni 5.7 kwa ajili ya ujenzi wa majosho 246 katika Halmashauri 63 nchi nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Kondoa Mjini jumla ya shilingi milioni 115,000,000 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa majosho matano katika kata za Kingale Mitaa ya Msui na Tampori, Serya Mtaa wa Chandimo, Suruke Mtaa wa Tungufu na Kondoa Mjini Mtaa wa Tumbelo chang’ombe. Hivyo basi, ninamshauri Mheshimiwa Mbunge kuwasiliana na kujadiliana na Mkurugenzi wa Halmashauri ili kama kuna haja ya mabadiliko ya maeneo ya ujenzi wa majosho yaweze kufanywa kulingana na vipaumbele vya wananchi na Halmashauri. Ahsante.