Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 51 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 667 2023-06-20

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuinusuru Benki ya Wakulima Mkoa wa Kagera ambayo ipo chini ya uangalizi wa BOT?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Oscar Ishengoma Kikoyo, Mbunge wa Muleba Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, mnamo tarehe 4 Januari, 2018 Benki Kuu ya Tanzania iliifutia leseni ya kufanya biashara Benki ya Wakulima Mkoa wa Kagera baada ya kushindwa kutimiza masharti ya leseni. Sambamba na uamuzi wa kuifutia leseni, Benki Kuu iliamua kuiweka benki hii chini ya ufilisi na iliiteua Bodi ya Bima ya Amana (Deposit Insurance Board - DIB) kuwa mfilisi wa benki hiyo. Kwa muktadha huo, iliyokuwa Benki ya Kagera Farmers’ Cooperative Bank Limited haipo chini ya uangalizi wa Benki Kuu ila ipo chini ya ufilisi wa DIB baada ya kufutiwa leseni ya biashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Sheria ya Benki na Taasisi za Fedha, 2006, benki ikishafutiwa leseni na kuwekwa chini ya ufilisi hakuna tena uwezekano wa benki kuendelea kuwepo na hivyo Serikali haina mpango wa kuifufua benki hiyo ila inafanya ufuatiliaji ili kuhakikisha kuwa zoezi la ufilisi linakamilika. Hadi Machi 2023, Bodi ya Bima ya Amana ilikuwa imelipa fidia ya bima ya amana jumla ya shilingi milioni 846.11 kwa wateja 1,389 waliokuwa na amana kwenye Benki ya Wakulima ya Kagera kati ya jumla ya shilingi milioni 899.56 zilizopaswa kulipwa kwa wateja 2,797 kulingana na matakwa ya sheria, ahsante.