Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 3 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 36 2016-09-08

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza:-
Kampuni ya BG-EXXON MOBIL, OPHIR na washiriki wenzao wako tayari kuanza ujenzi wa LNGPlant.
(a) Je, ni nini kinachokwamisha kuanza kwa utekelezaji wa mpango huo?
(b) Je, ni hatua gani za makusudi zinachukuliwa ili kuharakisha utekelezaji wa mradi huo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini napenda kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Dadi Chikota, Mbunge wa Nanyamba, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Mradi wa Kusindika Gesi Asilia (Liquefied Natural Gas – LNG) ulibuniwa mwaka 2014 kufuatiwa ugunduzi wa gesi asilia nchini ambao umetoka katika bahari ya kina kirefu. Mradi huo unatekelezwa katika na kampuni za kimataifa ya Statoil ya Norway, BG ya Uingereza, Exxon Mobil ya Marekani pamoja na Ophir ya Uingereza. Kampuni nyingine Pavilion ya nchini Singapore pamoja na shirika la TPDC ambalo ni la Serikali hapa nchini. Kutokana na umuhimu wa wa mradi huo katika kujenga uchumi wa gesi asilia nchini Serikali inachukua hatua za utekelezaji wa mradi kwa awamu tofauti. Lakini Serikali inachukua tahadhari muhimu sana katika kuandaa mradi huu.
Mheshimiwa Spika, napenda kulitaarifu Bunge lako Tukufu kuwa utekelezaji wa mradi huo unaendelea vizuri. Hatua zilizofikiwa kwa sasa ni pamoja na kupata eneo la LNG litakalojengwa kwa umbali wa kilometa 2,000 na katika eneo lingine ambalo litakamilika mpaka 2020.
Mradi huu unatekelezwa kama nilivyosema na TPDC ambapo kufikia mwaka 2015 Serikali ilikabidhi TPDC hatimiliki ya eneo ambalo kwa sasa tafiti mbalimbali za kihandisi, kijiolojia, kimazingira na kijamii zinaendelea kufanyika.
Mheshimiwa Spika, maandalizi ya mikataba mbalimbali yameanza baada ya Serikali kukamilisha uundaji wa timu ya kufanya majadiliano (government negotiating team). Majadiliano kati ya government negotiationteam yameanza na yatakamilika mwezi Septemba mwaka huu. Mahojiano hayo pamoja na mambo mengine yanafanya pia ifikapo mwaka 2020 kukamilika kwa ufasaha kabisa. Aidha, Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini hukutana na wawekezaji hao kila baada ya miezi mitatu ili kutathmini maendeleo ya utekelezaji wa mradi huu.