Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 3 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 35 2016-09-08

Name

Sophia Mattayo Simba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA M. SIMBA aliuliza:-
Hali ya magereza nchini ni mbaya hivyo kufanya vigumu katika utoaji wa haki za kibinadamu licha ya kwamba nchi imekuwa ikijali sana utekelezaji wa mikataba mbalimbali ya kikanda na ya kimataifa katika utoaji wa haki hizo za wafungwa.
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha hali hiyo katika magereza nchini?
(b) Je, Serikali imejenga magereza mapya mangapi katika kipindi cha miaka 20 iliyopita?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Sophia Mathayo Simba, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali ina mpango wa kuboresha hali ya magereza nchini kwa awamu kadri ya fedha zitakavyopatikana. Katika mwaka wa fedha 2016/2017 Serikali imetenga fedha katika fungu la maendeleo na matumizi mengineyo kwa ajili ya ukarabati, upanuzi, ujenzi wa mabweni mapya, majengo ya utawala na ununuzi wa vifaa mbalimbali vya malazi katika magereza nchini ili kuboresha huduma kwa mahabusu na wafungwa kukidhi vigezo vya haki za binadamu.
Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha miaka 20 iliyopita Serikali imejenga magereza mapya 11 kwa mchanganuo ufuatao:-
1. Gereza la Mkuza- 1996;
2. Gereza la Mbarali - 2003;
3. Gereza la Igunga - 2003;
4. Geeza la Meatu - 2003;
5. Gereza la Mgagao - 2004;
6. Gereza la Kinegele - 2005;
7. Gereza la Mbozi - 2005;
8. Gereza la Mbinga - 2007;
9. Gereza la Chato - 2008;
10. Gereza la Kiteto - 2009; na
11. Gereza la Karatu - 2010.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo magereza hayo pamoja na ujenzi kutokamilika yanaendelea kutumika isipokuwa Gereza la Chato na Gereza la Karatu.