Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 37 Good Governance Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 484 2023-05-31

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza:-

Je, lini Serikali itaweka wazi vigezo vya kubaini kaya maskini zinazostahili kupokea msaada wa TASAF?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejementi ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, naomba kumjibu Mheshimiwa Injinia Mwanaisha Ng’azi Ulenge, Mbunge wa Viti Maalam, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, vigezo vya utambuzi wa kaya za walengwa viko wazi na vinatambulika. Vigezo hivyo ni kama ifuatavyo ili kuweka record sawa katika Bunge lako:-

(i) Kaya ambazo hazina uwezo wa kupata kwa uhakika angalau milo miwili kwa siku;

(ii) Kaya isiyo na kipato cha uhakika na inayo wategemezi wengi wakiwemo watoto wanaokosa huduma za elimu na afya;

(iii) Kaya zinazoishi kwenye makazi duni yanayohatarisha usalama wa kaya;

(iv) Wazee wasio na msaada wowote;

(v) Watoto wanaoishi wenyewe bila wazazi au walezi.

Mheshimiwa Spika, vigezo hivi ndivyo vimewezesha Serikali kuweza kuhudumia kaya za walengwa 1,378,000 ambao wanaendelea kunufaika na mpango wa kunusuru kaya maskini (TASAF).