Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 28 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 233 2016-05-25

Name

Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. ZAINAB M. VULU (K.n.y MHE. ALLY S. UNGANDO) aliuliza:-
Kuendana na kasi ya Mheshimiwa Rais kutaka kumaliza kabisa urasimu wa upatikanaji wa hati za kimila na hati za ardhi mpaka sasa bado ni tatizo kwa Wilaya ya Rufiji:-
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Afisa Ardhi Mteule?
(b) Je, Serikali haioni kwamba ina kila sababu ya kupeleka vifaa vya kisasa vya kupima viwanja na mashamba?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Seif Ungando, Mbunge wa Jimbo la Kibiti, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kawaida, Afisa Mteule na ni Mwajiriwa katika halmashauri husika. Kabla ya kuteuliwa kuwa Afisa Ardhi Mteule, mapendekezo ya uteuzi huanzia katika halmashauri husika kutoa pendekezo ambalo linawasilishwa kwa Katibu Tawala wa Mkoa husika ambaye na yeye ataliwasilisha pendekezo hilo kwa Kamishna wa Ardhi. Pendekezo litakapowasilishwa kwa Kamishna wa Ardhi, Kamishna atafanya uteuzi wa Afisa Mteule Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji afuate utaratibu huo nilioueleza hapo awali ili halmashauri yake iweze kupata Afisa Mteule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali pia inatambua umuhimu wa kupima viwanja na mashamba hapa nchini. Kwa kutambua umuhimu huo, Serikali imekuwa ikiziagiza halmashauri kutenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya upimaji. Aidha, katika kukabiliana na changamoto ya upatikanaji wa vifaa hivyo, Wizara kupitia Benki ya Dunia ipo katika mchakato wa kununua vifaa vya upimaji ambavyo vitasambazwa katika Kanda nane za Wizara yangu ili halmashauri zote zilizopo ndani ya kanda hizo ziweze kunufaika.