Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 8 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 121 2023-09-07

Name

Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga jengo jipya la Mahakama ya Wilaya Nachingwea?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ninakushukuru na kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria naomba sasa nijibu swali la Mheshimiwa Tecla Mohamedi Ungele, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutekeleza mpango wa ujenzi na ukarabati wa majengo ya Mahakama katika ngazi mbalimbali ili kuboresha mazingira ya utoaji haki. Katika mpango huo Mahakama ya Wilaya ya Nachingwea imepangwa kujengwa katika mwaka huu wa fedha 2023/2024. Mshauri Elekezi ameshakamilisha usanifu na maandalizi ya gharama za mradi na taratibu za kupata Mkandarasi wa ujenzi zinaendelea.

Mheshimiwa Spika, jengo linatarajiwa kukamilika ifikapo Juni, 2024.