Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 8 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 118 2023-09-07

Name

Mwanakhamis Kassim Said

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Magomeni

Primary Question

MHE. MWANAKHAMIS KASSIM SAID aliuliza:-

Je, kwa nini Jeshi la Polisi haliondoi zuio la kuwahudumia wananchi wanaokwenda kupata huduma kwenye vituo nje ya maeneo yao?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwanakhamis Kassim Said, Mbunge wa Magomeni kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa kifungu cha 7 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai Namba 20 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2022, kikisomwa pamoja na Kanuni za Jeshi la Polisi (PGO) Namba 309, mtu yeyote aliyetendewa au anayefahamu jinsi kosa lilivyotendeka au linavyotaka kutendeka anatakiwa kutoa taarifa kituo chochote cha Polisi kilicho karibu na taarifa hiyo itachukuliwa na kufanyiwa kazi. Hivyo, hakuna zuio lolote la kuwahudumia wananchi wanaohitaji huduma za polisi kwenye vituo vilivyo nje na maeneo yao, nashukuru.