Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 28 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 232 2016-05-25

Name

Salma Mohamed Mwassa

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALMA M. MWASSA aliuliza:-
Kumekuwa na Migogoro mingi ya ardhi mjini na vijijini inayotokana na kutopima na kupanga matumizi bora ya ardhi:-
(a) Je, Serikali imejipangaje kupunguza au kumaliza migogoro ya ardhi?
(b) Je, lini Serikali itaandaa mipango Kabambe (Master plans) mijini na vijijini lili kuainisha matumizi bora ya ardhi na kuondoa migogoro ya ardhi nchini?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Salma Mohamed Mwassa, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla ya kujibu swali la Mheshimiwa Salma Mohamed Mwassa, Mbunge wa Viti Maalum, lenye vipengele (a) na (b), napenda kutoa maelezo mafupi ya vyanzo vya migogoro kama ifuatavyo:-
Utwaaji wa ardhi bila fidia stahiki; taasisi za umma na binafsi kuwa na maeneo au mashamba makubwa bila kuyaendeleza na kuyalinda; utata wa mipaka kati ya vijiji na wilaya pamoja na hifadhi; uvamizi wa viwanja na mashamba; kutokuwepo kwa mipango ya matumizi ya ardhi;ongezeko kubwa la idadi ya watu na shughuli mijini na vijijini katika ardhi ile ile na kutoheshimu sheria na mipango ya matumizi ya ardhi na shughuli za makundi ya watu wengine kama vile wakulima na wafugaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kupunguza na kutatua migogoro ya ardhi, Wizara imekuwa ikitekeleza mambo yafuatayo:-
(i) Kuandaa kitabu cha orodha ya migogoro ya Nchi nzima kinachoainisha vyanzo vyake ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa;
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI:
(ii) Kuwasiliana na Wizara zinazohusika na kilimo, mifugo na uvuvi; maliasili na utalii pamoja na TAMISEMI ili kutatua migogoro mtambuka;
(iii) Kuandaa matumizi ya ardhi katika vijiji na miji ambako migogoro ya ardhi imekuwa ikijitokeza na kusambaza miongozo inayohusu sera na sheria za ardhi;
(iv) Halmashauri zote nchini zimeelekezwa kuainisha viwanja na mashamba yasiyoendelezwa ipasavyo ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa;
(v) Kuimarisha mfumo wa ki-electronic katika kutunza kumbukumbu;
(vi) Kuimarisha ofisi za kanda ili kusogeza huduma za ardhi karibu na wananchi;
(vii) Kuanzisha Mfuko wa Fidia ya Ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu utayarishaji wa mipango kabambe ya miji, Wizara imekuwa ikitekeleza mambo yafuatayo:-
(i) Kuunda na kukamilisha program ya kupanga, kupima na kumilikisha kila kipande cha ardhi Tanzania itakayotekelezwa katika kipindi cha miaka 10 kuanzia mwaka 2015 mpaka 2025;
(ii) Wizara inasaidiana na Halmashauri za Wilaya na miji 18 kwenye program ya Urban Local Government Supporting Program katika utayarishaji wa mipango kabambe; na
(iii) Kujadiliana na Benki ya Dunia ili kuharakisha zoezi la utayarishaji wa mipango kabambe katika miji mingine 30 ya Tanzania bara.