Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 28 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 231 2016-05-25

Name

Emmanuel Papian John

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. JOHN aliuliza:-
Kwa kipindi kirefu sasa kumekuwa na migogoro mingi ya ardhi huko Kiteto baina ya wakulima na wafugaji:-
(a) Je, ni lini Serikali itaipatia Kiteto Mahakama ya Baraza la Ardhi ili kesi nyingi ziweze kusikilizwa hapo Kiteto?
(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kupima ardhi yote ya Kiteto ili kila mtu afahamu mipaka ya eneo lake ili kuepusha mwingiliano wa maeneo usio wa lazima, itafanya hivyo lini?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, naomba kujibu swali namba 231 la Mheshimiwa Emmanuel Papian John, Mbunge wa Kiteto, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijajibu naomba nifanye sahihisho dogo kwenye jibu la msingi isomeke mwaka 2015/2016 na siyo 2016/2017 kama ilivyoandikwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu sasa Wabunge wafahamu kuwa lengo la Serikali la kuunda Mabaraza ya Ardhi katika kila Wilaya ni kusogeza huduma za utatuzi wa migogoro karibu na wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2015/2016, Wizara iliahidi kuunda Mabaraza nane likiwemo Baraza Nyumba katika Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Kiteto ametoa jengo ambalo tayari limeshafanyiwa ukaguzi ili kubaini mahitaji. Wizara imekwisha nunua samani za ofisi na hata sasa inaendelea na taratibu za upatikanaji wa watendaji. Taratibu hizo zitakapokamilika baraza litaanza kazi mara moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sehemu ya pili, Novemba, 2014, kikosi kazi cha kushughulikia mipaka ya maeneo katika Wilaya ya Kiteto kiliundwa. Kikosi kazi hicho kilijumuisha wataalam kutoka Ofisi ya Rais, TAMISEMI; Ofisi ya Takwimu; Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na wataalam kutoka Halmashauri ya Kiteto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi zilizofanyika zilikuwa ni kurekebisha mipaka ya vijiji 10; Kijiji cha Loltepes, Emart, Enguserosidan, Kimana, Kinua, Nhati, Nemalock, Ndirigishi, Krashna na Taigo) katika eneo lililokuwa limegombewa kuzunguka hifadhi ya Emboley Murtangos kukamilisha mipango shirikishi ya matumizi bora ya ardhi katika vijiji 10 ni pamoja na kupima mashamba 2,110 katika vijiji vitatu, Kijiji cha Loltepes mashamba 385; Kimana mashamba 1,250; na Nemalock 475 na kutoa elimu iliyolenga kutatua migogoro ya ardhi katika Wilaya ya Kiteto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi hii ni kazi endelevu na itakamilika kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha.