Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 28 Works, Transport and Communication Ofisi ya Rais TAMISEMI. 229 2016-05-25

Name

Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE aliuliza:-
Serikali ilifanya tathmini na kuona umuhimu wa kujenga daraja kwenye Kata ya Ruhembe kwa shilingi milioni mia sita lakini mpaka sasa shilingi milioni 100 tu zimepelekwa kwenye Halmashauri ya Kilosa.
Je, ni lini kiasi cha shilingi milioni 500 kilichobakia kitapelekwa ili kukamilisha daraja hilo na kuwasaidia wananchi wa Ruhembe wanaozunguka umbali mrefu ili kupata mahitaji yao?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Leonard Haule, Mbunge wa Mikumi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha zilizoidhinishwa na Serikali katika bajeti ya mwaka 2014/2015, kwa ajili ya ujenzi wa daraja la Ruhembe zilikuwa ni shilingi milioni 300 fedha zilizopokelewa hadi Juni, 2015 zilikuwa shilingi milioni 100 ambazo zilitumika kwa ajili ya usanifu wa ujenzi wa daraja hilo. Mkandarasi aliyeomba fedha hizo anahitaji shilingi milioni 600 na hivyo kusababisha mradi huo kutotekelezeka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti ya mwaka 2016/2017, zimetengwa shilingi milioni 700 ambazo zitatumika kujenga daraja hilo na kuchonga njia inayounganisha daraja hilo.