Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 3 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 41 2023-08-31

Name

Janejelly Ntate James

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANEJELLY J. NTATE aliuliza: -

Je, lini Serikali itarekebisha Sheria za Utumishi zilizopitwa na wakati hasa kipindi hiki cha teknolojia?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijaanza kujibu swali la Mheshimiwa Janejelly James Ntate, naomba uniruhusu nitumie nafasi hii kumshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kuendelea kuniamini kuendelea kudumu katika Wizara hii ya Utumishi na Utawala Bora. Sasa naomba kujibi swali la Janejelly James Ntate.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Janejelly James Ntate, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua uwepo wa maendeleo makubwa ya kiteknolojia ambayo yamekuwa nyenzo muhimu katika kuimarisha utendaji kazi katika utumishi wa Umma. Ili kuendana na kasi ya mabadiliko ya teknolojia, Serikali imeendelea kufanya mapitio ya Mfumo wa Kisheria unaosimamia Utumishi wa Umma ambapo mwaka 2019 Serikali ilitunga Sheria ya Mamlaka ya Serikali Mtandao Namba10 ya Mwaka 2019 ili kuweka mazingira wezeshi ya matumizi ya teknolojia katika utendaji kazi wa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitishwa kwa Sheria hiyo kumeisaidia Serikali kuboresha utendaji kazi wake kupitia matumizi ya teknolojia. Pamoja na mambo mengine Sheria hiyo imewezesha kusanifiwa na kujengwa kwa jumla ya mifumo zaidi ya 860 ya TEHAMA Serikalini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na hatua za kupitia na kufanya marekebisho ya Sheria mbalimbali zinazosimamia Utumishi wa Umma na Kanuni zake ili kuhakikisha kwamba zinaendana na mabadiliko ya teknolojia.