Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 32 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 428 2023-05-24

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. ENG. SAMWELI X. HHAYUMA K.n.y. MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kupeleka mbegu za mahindi kabla ya kipindi cha masika katika Jimbo la Mbulu Vijijini?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Gregory Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mpango wa kuwafikishia wakulima pembejeo za kilimo kwa wakati ikiwemo mbegu bora za mahindi katika Jimbo la Mbulu Vijijini na maeneo mengine nchini unahusisha kukusanya takwimu za mahitaji halisi na kuratibu usambazaji wa pembejeo hizo kupitia sekta ya umma na sekta binafsi kabla ya msimu wa kilimo kuanza.

Mheshimiwa Spika, katika msimu wa mwaka 2022/2023 na mwaka 2023/2024 Serikali kupitia Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA) ambayo ni Taasisi ya Serikali imeendelea kusambaza mbegu bora za mahindi katika maeneo mbalimbali kwa bei nafuu ambayo ina ruzuku ndani yake. Ninaomba nitumie fursa hii kupitia Bunge lako Tukufu kuzishauri Halmashauri za Wilaya ikiwa ni pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu kutenga fedha zitakazowezesha kuendelea kununua mbegu za mahindi pamoja na mbegu za mazao mengine kupitia Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA) ambao huuza mbegu kwa bei nafuu zaidi.