Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 32 Investment and Empowerment Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 427 2023-05-24

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kutoa mwongozo kwa wawekezaji kuchangia shughuli za maendeleo katika maeneo wanayowekeza?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Michael Costantino Mwakamo, Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha wawekezaji wanachangia shughuli za maendeleo za jamii katika maeneo wanayowekeza, Serikali ina sheria za kisekta na miongozo inayosimamia wawekezaji katika sekta ya uziduaji ambayo ni mwongozo wa ushiriki wa Watanzania katika sekta ndogo ya mafuta 2019, mwongozo wa kuwasilisha mpango wa ushiriki wa Watanzania katika sekta ya madini wa mwaka 2018 na mwongozo kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhusu uwajibikaji kwa jamii wa makampuni wa mwaka 2022. Aidha, Serikali iliandaa mwongozo wa Taifa wa ushiriki wa Watanzania katika sekta mbalimbali wa mwaka 2019 kwa ajili ya kusimamia masuala ya ushiriki wa Watanzania katika miradi ya kimkakati na uwekezaji. Utaratibu huo unaruhusu wawekezaji kuchangia sehemu ya mapato yake kwa jamii ikiwa ni sehemu ya uwajibikaji kwa jamii na kuchangia shughuli za maendeleo katika eneo la uwekezaji kupitia Mamlaka za Serikali za Mitaa. Nakushukuru.