Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 32 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 426 2023-05-24

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza: -

Je, nini mpango wa Serikali kuingiza lugha ya alama kwenye mitaala ya elimu nchini?

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) K.n.y WAZIRI WA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stella Ikupa Alex, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inao mpango wa kuingiza lugha ya alama kwenye mitaala ya elimu nchini kwa lengo la kutatua changamoto ya mawasiliano kwa wanafunzi viziwi na katika jamii. Aidha, katika mchakato wa mapitio ya sera ya mitaala unaoendelea somo la Lugha ya Alama limependekezwa liwe la lazima kwa walimu wote tarajali katika vyuo vyote vya ualimu na vyuo vikuu nchini.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kuwepo kwa mpango na mapendekezo hayo, tayari Serikali imeandaa na kusambaza kamusi ya lugha ya alama ya Tanzania ya kidijitali katika shule na vyuo vinavyopokea wanafunzi viziwi. Aidha, kozi ya lugha ya alama ya Tanzania inatolewa katika Chuo cha Ualimu Patandi na Kabanga na katika Vyuo Vikuu vya Dodoma, Dar es Salaam na Archbishop Mihayo University College Tabora kwa lengo la kumudu darasa jumuishi. Aidha, Serikali imeendelea kutoa mafunzo kwa walimu maalum na wasio wa elimu maalum 3,650 wa shule za msingi na sekondari kwa lengo la kuwajengea uwezo wa namna bora ya kuwafundisha na kuwahudumia wanafunzi viziwi ili kujenga jamii jumuishi ya viziwi shuleni.