Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 32 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 424 2023-05-24

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga angalau kilometa tano kwa kiwango cha lami Barabara ya Tunduru - Mtwara Pachani?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Zidadu Kungu, Mbunge wa Tunduru Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza ujenzi wa barabara ya Mtwara Pachani – Lusewa – Lingusenguse – Nalasi hadi Tunduru yenye urefu wa kilometa 300 kwa awamu ambapo jumla ya kilometa 3.23 zimejengwa kwa lami nyepesi katika maeneo ya miji midogo ya Mkongo, Ligela, Lusewa na Sasawala. Aidha, mwezi Machi, 2023 Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imesaini mkataba kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa kipande cha mita 500 katika eneo la Tunduru Mjini. Vile vile, Serikali imekamilisha kazi ya Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara hii.

Mheshimiwa Spika, baada ya Usanifu kukamilika Serikali inaendelea kutafuta fedha za kuendelea na ujenzi, ahsante.