Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 32 Water and Irrigation Wizara ya Maji 422 2023-05-24

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: -

Je, lini fedha itatengwa kufanya usanifu na upembuzi yakinifu wa Mradi wa kutoa maji Ziwa Nyasa kupeleka Tarafa ya Masasi – Ludewa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Zacharius Kamonga, Mbunge wa Ludewa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Tarafa ya Masasi Wilaya Ludewa ina jumla ya vijiji 15, ambapo vijiji 12 vinapata huduma ya maji na vijiji viwili vya Igalu na Kiyogo utekelezaji wa miradi unaendelea na unatarajia kukamilika mwezi Juni, 2023.

Mheshimiwa Spika, mojawapo ya vipaumbele vya Wizara kwa mwaka 2023/2024 ni kusanifu na kutekeleza miradi ya maji kwa kutumia vyanzo vya uhakika ikiwemo maziwa makuu, kupeleka maji kwenye maeneo yenye uhaba pamoja na vijiji vilivyomo pembezoni mwa maziwa hayo. Kwa upande wa Ziwa Nyasa, fedha za awali zimeshatengwa kwa ajili ya usanifu na tathmini ya athari za kimazingira na kijamii ambapo vijiji vya Tarafa ya Masasi Wilayani Ludewa vitanufaika na miradi ya maji kupitia chanzo hicho.