Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 32 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 421 2023-05-24

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA K.n.y. MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha usajili wa Shirikisho la International Federation of Cross and Crescent nchini?

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI) K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria naomba kujibu swali la Mheshimiwa David Mwakiposa Kihenzile Mbunge wa Mufindi Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Shirikisho la Kimataifa la Msalaba Mwekundu (International Federation of Red Cross and Crescent - IFRC) ni Shirika la Kimataifa linalounganisha vyama vya nchi mbalimbali vya Msalaba Mwekundu. Nchini Tanzania Chama cha Msalaba Mwekundu kilianzishwa chini ya Sheria Na. 71 mwaka 1962 kufuatia nchi yetu kuridhia mikataba ya Geneva yam waka 1949. Kazi kubwa ya Shirikisho hili ni kufanya shughuli za kusaidia wahanga wa maafa na kuimarisha uwezo wa wanachama wake katika kukabiliana na maafa. Kutokana na umuhimu wa Shirikisho hilo kwa nchi yetu, tayari Serikali imekamilisha majadiliano na uongozi wa IFRC na zoezi la kuwashirikisha wadau wote wanaohusika hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa, Serikali iko katika hatua za mwisho kukamilisha mkataba na shirikisho hilo, hatua hizo zitakapokamilika mkataba utasainiwa na Ofisi za IFRC kufunguliwa nchini na kuanza kufanya kazi. Ahsante.