Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 32 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 417 2023-05-24

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga miundombinu ya maji mashuleni ili kuepusha milipuko ya magonjwa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ghati Zephania Chomete, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuhakikisha kuwa shule zote za Msingi na Sekondari zinakuwa na miundombinu ya maji safi na salama pamoja na vifaa vya kunawia mikono vikiwemo ndoo, jaba tiririka na miundombinu iliyojengwa kwa pamoja (mass handwashing facilities). Aidha, katika mwaka wa fedha wa 2022/2023 Serikali kupitia mradi wa usafi na mazingira (SRWSS) imejenga miundombinu bora ya kunawia mikono pamoja na vifaa vya kuhifadhia maji katika shule za msingi 1853.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuhamasisha usafi mashuleni kupitia vilabu vya uhamasishaji usafi mashuleni (Swash Clubs).