Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 5 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 53 2016-02-01

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza:-
Serikali imeshaweka Mkandarasi ambaye kwa sasa yuko site anaendelea na kazi ya Mradi wa umeme katika Vijiji vya Mawande-Utengule, Luhota, Ngamanga, Ikwata, Mlowa, Mkolanga, Ibumila, Mahongole, Manga Usetule, Kifumbe, Mtanga, Kitandililo, Ibatu, Nyamande, Mtulingala na Mbugani;
Je, ni lini mradi huo wa umeme katika vijiji hivyo utakamilika?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Deo Kasenyanda Sanga, Mbunge wa Makambako, kama ifuatavyo:-
Ni kweli kwamba Serikali imeweka Mkandarasi Lucky Exports ambaye kwa sasa anatekeleza mradi wa REA awamu ya pili Mkoani Njombe. Mkandarasi huyo amepewa Vijiji vya Ikwata, Kifumbe, Luhota, Manga, Mlowa, Mwande, Ngamanga, Usetule pamoja na Utengule, ambayo amepatiwa kama kazi ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kazi ya usanifu tayari imekamilika na kwa sasa Mkandarasi anasubiri kusaini Mkataba kati yake na Wakala wa Umeme Vijijini (REA) kabla ya mwezi Machi mwaka huu, ili aanze utekelezaji wa mradi. Kazi ya kupeleka umeme katika vijiji hivi unajumuisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilomiti 38.8, lakini pia ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilomita 51, ufungaji wa Transfoma 19 ambapo transforma nne za ukubwa wa kVA 25 na transfoma 15 za ukubwa kwa kVA50. Hii ni pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 1,875. Kazi hii itachukua miezi sita kukamilika na itagharimu shilingi bilioni 3.3.
Mheshimiwa Spika, Vijiji vya Mahongole, Manga, Mbugani, Mtanga, Mtulingala, na Nyamande vimewekewa umeme kwenye Mradi wa awamu ya tatu, (REA phase III) inayoanza utekelezwa hivi karibuni. Kazi ya kupeleka umeme kwenye Vijiji hivi inajumuisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33, yenye urefu wa kilomita 73, ujenzi wa njia ya umeme wa msongo kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilomita 36, ufungaji wa transfoma 14 ambapo transfoma tano za ukubwa wa kVA 25 na transfoma tisa za ukubwa wa kVA 50. Hii ni pamoja na kuwaunganishia umeme wateja awali 1493. Kazi hii itaanza Julai mwaka huu na itagharimu shilingi bilioni 4.05.
Mheshimiwa Spika, Vijiji vya Ibatu, Ibumila na Kitandililo tayari vimefanyiwa tathmini ya gharama za kupeleka umeme na kazi inatakiwa kufanyika kwenye kazi za nyongeza lakini kutokana na gharama kuwa kubwa itajumuishwa kwenye mradi wa awamu ya tatu.
Mheshimiwa Spika, kazi ya kupeleka kwenye vijiji hivi inajumuisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu kilomita 11, ujenzi wa njia ya umeme wa msongo kilovoti o.4 yenye urefu wa kilomita 13 pamoja na ufungaji wa transfoma tano ambapo transfoma ambapo transfoma moja ina ukubwa wa kVA 50 na transfoma Nne za ukubwa kVA 100.
Hii pia itaunganisha pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 589. Kazi hii itaanza Julai, 2016 na itagharimu takribani shilingi milioni 885.