Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 1 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 7 2016-09-06

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA aliuliza:-
Kila jamii ina mila na desturi zake; hapa nchini wanamuziki wamekuwa hawavai mavazi ya staha au utu wa mwanamke umekuwa ukidhalilishwa kutokana na kuvaa nguo zinazoonesha maungo yao.
Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti mavazi yasiyo na staha kwa wanamuziki wa kike?

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Mary Machuche Mwanjelwa, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Wizara yangu kupitia Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) imekuwa ikitoa elimu kwa wasanii mara kwa mara kupitia vyombo vya habari, makongamano, semina na warsha juu ya umuhimu wa maadili katika sanaa na namna ya kubuni kazi za sanaa zenye ubora na zinazozingatia maadili, elimu imekuwa ikitolewa kupitia vyombo mbalimbali vya habari ikiwemo E fm Radio, EATV, Magic FM, Azam TV, Channel Ten, Clouds Entertainment na TBC.
Mheshimiwa Spika, kwa wasanii wanaokiuka maadili kwa kuvaa mavazi au kubuni kazi za sanaa zinazomdhalilisha mwanamke hatua za kinidhamu na kisheria kama vile kufungia kazi zao, kuwafungia wao wenyewe na kuwatoza faini zimekuwa zikichukuliwa.
Mheshimiwa Spika, kuanzia mwaka 2014/2015 mpaka sasa wasanii watatu wa kike na msanii mmoja wa kiume na kikundi kimoja cha kanga moko walipewa maonyo na wengine kufungiwa kabisa kwa kudhalilisha utu wa mwanamke. Aidha,kwa mwaka 2016/2017 msanii mmoja wa kiume alipewa onyo na kutozwa faini.
Mheshimiwa Spika, Sera ya Taifa ya Utamaduni ya mwaka 1997 imeeleza wazi kwamba kila Mtanzania ana wajibu wa kulinda mila na desturi zetu sambamba na kuhakikisha maadili yanalindwa na mwanamke hadhalilishwi wakati wa shughuli za sanaa. Wizara yangu inapenda kutoa wito kwa kila Mtanzania kuhakikisha kwa namna moja au nyingine anatunza na kulinda maadili na utamaduni wa Mtanzania.