Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 24 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 213 2022-05-17

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: -

Je, Serikali inachukua hatua gani kukomesha kuvuja kwa mitihani nchini?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Husna Juma Sekiboko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kwa lengo la kukomesha tabia ya udanganyifu katika mitihani ya Taifa ikiwemo mitihani ya kumaliza elimu ya msingi, sekondari na vyuo. Hatua hizo ni pamoja na kutoa elimu kwa walimu, wasimamizi wa mitihani na wadau wote wa elimu kuhusu athari za udanganyifu katika mitihani ili kuhakikisha kuwa wanatekeleza jukumu la usimamizi wa mitihani hiyo kwa uadilifu na kwa kuzingatia kanuni, taratibu na miongozo iliyowekwa kwa ajili ya uendeshaji wa mitihani.

Mheshimiwa Spika, hatua nyingine zilizochukuliwa kutokana na udanganyifu katika mitihani ni hatua za kinidhamu kwa mujibu wa sheria za nchi. Hatua hizi zimekuwa zikichukuliwa kwa Walimu, wasimamizi na wadau wote wanaohusika katika kusimamia mitihani pale ambapo ilibainika pasina shaka kuwa walishiriki katika kosa hilo.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuwachukulia hatua kali kwa mujibu wa sheria wahusika wote wanaojihusisha na udanganyifu wa mitihani ili kuhakikisha kuwa nchi inapata wataalam wenye sifa stahiki. Nakushukuru sana.