Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 24 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 212 2022-05-17

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE AIDA J. KHENANI K.n.y. MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: -

Je, kwa nini Serikali isitumie mbao za Mitiki zenye ubora sawa na Mninga/Mkongo kwani tenda za Serikali zinataka Mninga/Mkongo?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Naghenjwa Livingstone Kaboyoka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, shughuli za ujenzi na utengenezaji wa samani ambazo kiuhalisia zimekuwa zikikua sambamba na ongezeko la watu, zinategemea sana rasilimali ya misitu kama chanzo cha malighafi.

Mheshimiwa Spika, kutokana na kukua kwa mahitaji na changamoto ya upatikanaji wa miti migumu kutoka katika misitu ya asili hasa jamii ya mninga na mkongo, Wizara imefanya utafiti kuhusu tabia na sifa za mbao za matumizi kutoka kwenye miti isiyofahamika sana. Utafiti huo uliolenga kutambua tabia na sifa za kimwonekano, kiufundi na kianatomiki za mbao za miti isiyojulikana sana, ulionesha kuwa mti wa mitiki, una sifa ama sawa au zinazokaribiana sana na miti ya mkongo na mninga.

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia matokeo ya utafiti huo, Serikali inaangalia uwezekano wa kuongeza miti mipya iliyofanyiwa utafiti katika orodha ya miti iliyoainishwa katika Sheria ya manunuzi inayosimamiwa na PPRA ili itumike katika kutengeneza samani za Serikali.