Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 2 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 30 2023-04-05

Name

Mariam Madalu Nyoka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM M. NYOKA aliuliza: -

Je, Serikali haioni umuhimu wa kununua gari la utawala na gari la Mganga Mfawidhi katika Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mariam Madalu Nyoka, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mhehsimiwa Spika, Serikali imenunua magari 727 kwa ajili ya kubebea wagonjwa na magari 146 kwa shughuli za kiutawala. Hadi sasa magari 20 yamepokelewa na magari 117 yapo njiani kutoka kwa mtengenezaji.

Mheshimiwa Spika, magari yote yanatarajiwa kuwasili nchini na kukabidhiwa katika vituo vya kutolea huduma kabla ya mwezi Juni 2023. Aidha, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa Hospitali zitakazopata mgao wa magari hayo.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.