Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 2 Investment and Empowerment Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 27 2023-04-05

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya uendeshaji wa Mabaraza ya Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, nakushukuru na kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Subira Khamis Mgalu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikiendesha Majukwaa ya Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi tangu mwaka 2017. Lengo kuu la majukwaa hayo ni kuwakutanisha wanawake ili waweze kujadili fursa za kiuchumi na changamoto mbalimbali wanazokutana nazo wakati wa utekelezaji wa shughuli za kiuchumi nchini.

Mheshimiwa Spika, hadi kufikia mwaka 2021/2022, mikoa yote 26 imezindua majukwaa ya wanawake katika halmashauri 140 kati ya halmashuri 184 na kata 1,149 kati ya kata 2,404. Lakini pia mitaa na vijiji 1,776 kati ya mitaa na vijiji 7,613.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2022/2023, Serikali ilitenga fedha zaidi ya milioni 72 na katika mwaka wa fedha unaokuja 2023/2024, Serikali imetenga shilingi milioni 200 kwa ajili ya uendeshaji wa majukwaa hayo.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.