Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 2 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 25 2023-04-05

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: -

Je, ni kwa nini Serikali haijagawa fedha kwa ajili ya ufugaji wa vizimba vya samaki katika Ziwa Nyasa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jacqueline Ngonyani Msongozi, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Ruvuma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ili kufuga samaki kwa vizimba inabidi kuainisha maeneo yanayofaa ziwani kwa kuzingatia vigezo vya kisheria na kitaalam. Katika awamu ya kwanza Serikali ilitoa fedha katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa Victoria ambayo ilishakidhi vigezo vya kisheria na kitaalam baada ya kufanyiwa tathmini katika Mwaka wa Fedha 2021/2022 na 2022/2023.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2023/2024, Serikali kupitia Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi (TAFIRI) imepanga kufanya tathmini ya kimkakati ya mazingira (Strategic Environmental Assessment) katika Ziwa Nyasa ili kuanisha maeneo yanayofaa kwa ufugaji wa samaki kwa vizimba kwa kuzingatia vigezo vya kisheria na kitaalam. Pia (TAFIRI) itaanza ufugaji samaki kwa majaribio kwa kushirikiana na wananchi kufanya uzalishaji wa vifaranga vya samaki aina ya magege (Oreochromis karongae) na ufugaji wake kwa vizimba. Hatua hii inalenga kuwajengea uwezo wananchi ili waweze kuendelea na ufugaji pindi taratibu zitakapokamilika.