Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 2 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 20 2023-04-05

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA K.n.y. MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: -

Je, hali ya upatikanaji wa vitabu vya kufundishia na kujifunza katika shule za msingi na sekondari ipoje?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna Salum Mtanda, Mbunge Wa Newala Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha uandishi, uchapaji na usambazaji wa vitabu vya kiada na viongozi vya mwalimu kwa masomo yote ya elimu ya awali na msingi darasa la I – VII. Vitabu hivyo ni pamoja na vitabu vya kiada vilivyotafsiriwa kwa ajili ya shule zinazotumia Kiingereza kama lugha ya kufundishia. Vitabu vya kiada vya wanafunzi walio nje ya mfumo rasmi (Mpango wa Elimu ya Msingi kwa Waliokosa – MEMKWA), vitabu vya kiada vya breli kwa wanafunzi wasioona na vitabu vilivyokuzwa maandishi kwa ajili ya wanafunzi wenye uoni hafifu. Aidha, imekamilisha kuandika, kuchapa na kusambaza jumla ya vitabu vya kiada vya masomo 171 kati ya 183 ya sekondari ikiwemo vitabu vya masomo ya sayansi, hisabati, sanaa, lugha, biashara, kilimo, michezo, muziki na vitabu vya ufundi ambavyo vipo hatua ya uchapaji. Vitabu 12 vilivyobaki ni vya masomo chaguzi (optional subjects) ikiwemo Kichina ambavyo vinatarajiwa kukamilika mwezi Juni 2023.

Mheshimiwa Spika, kutokana na jitihada hizo, hali ya upatikanaji wa vitabu, kwa shule za msingi na sekondari imefikia uwiano wa kitabu kimoja kwa wanafunzi watatu.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.