Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 17 2023-04-05

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza: -

Je, ni lini mfumo wa utawala wa Serikali za Mitaa utaanza kufanya kazi katika Kambi za Wakimbizi Mishamo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Moshi Selemani Kakoso, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Makazi ya Wakimbizi ya Mishamo yaliyopo Mkoa wa Katavi, Wilaya ya Tanganyika yalisajiliwa rasmi mwaka 1979. Baada ya usajili, Shirika la Dini la Tanganyika Christian Refugee Services lilipewa jukumu la kusimamia Makazi hayo na kutoa huduma za kijamii ikiwa ni pamoja na kufanya mpango wa kugawanya mitaa. Kupitia Mpango huo ilipatikana mitaa 21 iliyotambuliwa kwa namba kutoka mtaa namba 1 hadi 21.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa mitaa hiyo inatambulika kama vijiji baada ya wakazi hao kutumia majina badala ya namba zilizosajiliwa awali. Aidha, kuanzia Mwaka 1980 Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la UNHCR imekuwa ikitoa huduma za kijamii ikiwemo ujenzi wa shule, zahanati na barabara katika Makazi ya Wakimbizi Mishamo.

Mheshimiwa Spika, Maeneo haya yanaendelea kutambulika kupitia Gazeti la Serikali namba 537 la tarehe 19/07/2019. Aidha, Maeneo hayo bado yapo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na mara yatakapokabidhiwa Ofisi ya Rais TAMISEMI mfumo wa Utawala wa Serikali za Mitaa utaanza kufanya kazi.