Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 32 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 261 2016-05-30

Name

Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Primary Question

Kwa mujibu wa Ibara ya 45(1)(a) na (d) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano Rais anayo mamlaka ya kutoa msamaha kwa wafungwa waliopo magerezani.
Je, Rais anayo mamlaka kisheria ya kutoa msamaha kwa watuhumiwa wa uhalifu wa aina yoyote ambao mashauri yao yapo katika vyombo vya dola kwenye hatua za uchunguzi/upelelezi au mahakamani?

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Khatib Said Haji, Mbunge wa Konde kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Ibara ya 45(1)(a) mpaka (d) inampa Rais mamlaka ya kwanza kutoa msamaha kwa mtu yeyote aliyepatikana na hatia mbele ya mahakama, pili kumuachilia kabisa au kwa muda maalum mtu yeyote aliyehukumiwa au kuadhibiwa kwa ajili ya kosa lolote, tatu, kubadilisha adhabu yoyote aliyopewa mtu yeyote kwa kosa lolote iwe adhabu tahafifu na nne kufuta adhabu yoyote au sehemu ya adhabu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuzingatia masharti hayo ya Katiba msamaha wa Rais unatolewa kwa mtu aliyetiwa hatiani na kupewa adhabu na mahakama. Watuhumiwa wa uhalifu ambao mashauri yao yako katika hatua ya upelelezi au uendeshaji mahakamani hawaguswi na masharti ya ibara hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu hiyo basi, Rais hawezi kisheria kutoa msamaha kwa watuhumiwa wa uhalifu wa aina yoyote ambao mashauri yao yapo katika vyombo vya dola kwenye hatua za uchungu, upelelezi au mahakamani. Hatma ya watuhumiwa hao inakuwa bado ipo katika mamlaka husika za uchunguzi, mashitaka na mahakama.