Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 22 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 194 2022-05-13

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kukuza utalii wa fukwe za bahari nchini?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tunza Issa Malapo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kubuni mikakati mbalimbali ya kuendeleza Mazao mbalimbali ya Utalii, ikiwemo Utalii wa FUKWE. Katika kutekeleza mikakati hiyo, Idadi ya Watalii wanaotembelea fukwe zetu zilizopo katika mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Pwani, Lindi na Mtwara imeendelea kuongezeka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sambamba na hilo, Serikali imetekeleza yafuatayo: -

i. Kwanza ni kubaini maeneo mapya ya fukwe za Bahari ya Hindi yanayofaa kwa ajili ya uwekezaji wa shughuli za utalii katika Mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Pwani, Lindi na Mtwara;

ii. Lakini pia kuweka utaratibu wa kusajili maeneo ya fukwe yanayofaa kwa shughuli za Utalii kama Maeneo Maalum ya Uwekezaji wa Shughuli za Utalii (Tourism Special Economic Zone); na

iii. Lakini la mwisho ni kuendelea kuwahamasisha wamiliki wa maeneo ya fukwe nchini ili kusajili maeneo ya fukwe wanayoyamiliki chini ya utaratibu wa Maeneo Maalum ya Uwekezaji wa Shughuli za Utalii kwa lengo la kuiwezesha Serikali kushirikiana na wamiliki hao kuhimiza uwekezaji wa utalii wa fukwe.