Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 22 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 193 2022-05-13

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itazuia Mamba wanaoua watu na kujenga uzio wa nondo maeneo ambayo watu huchota maji Jimboni Buchosa?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Eric James Shigongo Mbunge wa Jimbo la Buchosa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwepo na matukio mbalimbali ya wanyama wakali kujeruhi au kusababisha vifo vya watu pembezoni mwa maeneo yenye maziwa, mito na mabwawa hususani mamba. Katika kukabiliana na changamoto hizo, Serikali inaendelea kutekeleza Mkakati wa Kitaifa wa Kusimamia Migongano baina ya Binadamu na Wanyama wakali na waharibifu. Aidha, kuanzia kipindi cha Julai, 2021 hadi Aprili, 2022 jumla ya mamba wawili wamevunwa katika Kata ya Maisome Wilayani Buchosa. Vilevile, katika kipindi tajwa watu 992 wamepewa elimu kuhusu namna ya kuepuka madhara ya wanyama wakali na waharibifu. Hadi sasa kikosi cha Askari wa Uhifadhi watatu wapo uwandani wanaendelea na doria za kudhibiti mamba katika Wilaya ya Buchosa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazishauri Mamlaka ya Serikali za Mtaa (Halmashauri) kuandaa mpango madhubuti wa kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa vizimba na Wizara ya Maliasili na Utalii itatoa wataalam.