Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 22 Works, Transport and Communication Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 192 2022-05-13

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Minara katika maeneo yasiyo na minara na kutatua matatizo ya mawasiliano katika maeneo yenye Minara?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta Mbunge wa Urambo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) inatekeleza miradi ya kufikisha huduma za mawasiliano katika kata tatu za Ugalla, Itundu na Vumilia Wilayani Urambo ambapo ujenzi wa minara unaendelea na utakamilika ifikapo Julai 2022.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali pia imepanga kufikisha huduma za mawasiliano ya simu Kata za Kiloleni, Kasisi, Itundu na Uyogo katika mwaka wa fedha wa 2022/ 2023 baada ya kubaini uwepo wa changamoto za mawasiliano katika baadhi ya maeneo ya vijiji katika kata hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kata hizo zimejumuishwa katika zabuni inayotarajiwa kutangazwa kabla ya mwaka wa fedha wa 2021/2022 kukamilika kupitia Mradi wa Tanzania ya Kidijitali. Utekelezaji wa miradi hii ya usimikaji wa minara ya mawasiliano utahusisha uboreshaji wa mawasiliano ili kukidhi mahitaji ya upatikanaji wa huduma za intaneti katika Kata za Songambele na Imalamakoye asante.