Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 19 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 165 2022-05-10

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: -

Je Serikali ina mkakati gani wa kushughulikia soko la ndani la maziwa kwa kuhimiza na kuhamasisha unywaji wa maziwa shuleni kabla ya kutafuta masoko ya nje?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bryceson Magessa Tumaini, Mbunge wa Busanda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea na mkakati wa kukuza soko la maziwa nchini kwa kuimarisha na kuendeleza programu mbalimbali zinazochochea unywaji wa maziwa ikiwemo programu ya unywaji wa maziwa shuleni. Mpango wa unywaji maziwa shuleni umeweza kuwafikia watoto 90,000 wa shule za msingi 39 katika Mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Iringa, Mbeya, na Tanga.

Vilevile Serikali inaendelea kuhamasisha unywaji maziwa nchini, kwa kutoa elimu kupitia vyombo vya habari, maonesho mbalimbali ya Wiki ya Maziwa Kitaifa inayoadhimishwa mwezi Mei kila mwaka.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali itakutana na wadau mbalimbali wakiwemo wa tasnia ya maziwa ili kuandaa mikakati thabiti kwa lengo la kuongeza idadi ya shule zinazotoa huduma ya unywaji wa maziwa. (Makofi)