Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 19 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 164 2022-05-10

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaitengea bajeti barabara inayounganisha Uganda na Tanzania ya Kibaoni - Kakunyu kwenda Bugango mpakani ambayo iko chini ya TARURA wakati taratibu za kupandishwa hadhi zikiendelea ili iweze kupitika wakati wote?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Florent Laurent Kyombo, Mbunge wa Nkenge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hiyo ya Kakunyu - Bugango ni muhimu kwa kuwa inaungaisha Nchi jirani ya Uganda pia hutumika katika kukuza shughuli za kiuchumi kwa wananchi wa Missenyi.

Mheshimiwa Spika, kwa kutambua umuhimu huo, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA), kwa mwaka wa fedha 2021/2022 ilitenga jumla ya Shilingi Million 41.08 kwa ajili ya matengenezo ya barabara hiyo katika maeneo korofi yenye urefu wa kilomita 3.0 na kazi hiyo imefanyika na kukamilika.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, Serikali imeendelea kuona umuhimu wa kuhakikisha kuwa wananchi wa Missenyi wanaweza kufika katika mpaka wa Bugango kwa kutenga jumla ya Shilingi Milioni 34.92 katika mwaka wa fedha 2021/2022 kwa ajili ya matengenezo ya barabara nyingine iliyopo jirani iitwayo Missenyi Ranchi - Bugango jumla ya kilomita 17.3 ambapo Mkandarasi yupo eneo la kazi anaendelea ukamilishaji wa matengenezo hayo. (Makofi)