Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 19 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 161 2022-05-10

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. SAPUTU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Jengo la Wagonjwa wa Nje, Jengo X-Ray, Jengo la Watoto na Jengo la Utawala katika Hospitali ya Wilaya Olturumet Halmashauri ya Arusha?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Noah Lemburis Saputu Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Ofisi ya Rais- TAMISEMI mwezi Aprili, 2021 ilipokea maombi maalum ya shilingi milioni 800 kwa ajili ya upanuzi na ukarabati wa Hospitali ya Olturumet ambayo miundombinu yake imechakaa.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga shilingi bilioni 16.55 kwa ajili ya ukarabati wa Hospitali Kongwe 19 nchini. Aidha, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali itaendelea kutafuta fedha kwa awamu kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa Hospitali Kongwe nchini ambapo Hospitali ya Olturumet itapewa kipaumbele.