Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 16 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 138 2022-05-05

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali italipa fidia wananchi waliotwaliwa ardhi yao kwa ujenzi wa viwanda maeneo ya Liganga na Mchuchuma?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa uwekezaji Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Zacharius Kamonga, Mbunge wa Ludewa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mradi Unganishi wa Mchuchuma na Liganga unatarajiwa kutekelezwa kwa ubia kati ya Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) kwa niaba ya Serikali na Kampuni Binafsi, ambaye ni mbia. Katika kutekeleza mradi huo, Serikali imetenga fedha katika bajeti ya mwaka 2022/2023 kwa ajili ya kufanya uthaminishaji upya na hatimaye kulipa fidia kwa wananchi wanaopisha mradi huo kwa mujibu wa Sheria.