Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 16 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 134 2022-05-05

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: -

Je, nini mpango wa Serikali katika kuharakisha kesi za mauaji ambazo huchukua muda mrefu kusikilizwa?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Edwin Enossy Swalle, Mbunge wa Lupembe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara yangu kupitia Ofisi ya Taifa ya Mashtaka imeunda kikosi kazi kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai cha kupitia majalada ya kesi za mauaji zenye muda mrefu kuanzia miezi miwili na kuendelea. Majalada hayo yanafanyiwa mapitio na kutolewa uamuzi. Kikosi kazi hiki kinaendelea na kazi ya kupitia majalada ambapo kazi hii inatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Mei, 2022.

Mheshimiwa Spika, nimwombe Mheshimiwa Mbunge kuwa na subira ili kutoa muda hadi mwishoni mwa mwezi Mei, 2022; kesi zote za muda mrefu zitakuwa zimeshughulikiwa.